Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 73 2022-04-20

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga walau KM Tatu za barabara ya lami katika Mji wa Laela - Sumbawanga ambao hauna barabara ya lami?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu Mbunge wa Jimbo la Kwela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Ujenzi wa barabara za lami katika Mji mdogo wa Laela ambazo zitachochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa Wananchi wa Mji huo. Aidha, katika Mwaka wa Fedha 2022/ 2023 Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini inatarajia kufanya zoezi la kuainisha na kuzifanyia usanifu barabara zenye urefu wa kilomita Tatu kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hizo ili kupata gharama halisi za ujenzi.

Mheshimiwa Spika, baada ya utambuzi na usanifu wa barabara hizo kukamilika, TARURA itaweka katika vipaumbele vyake barabara hizo kwa ajili ya kuanza ujenzi katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024.