Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga skimu katika vijiji vya Maore, Mpirani, Kadando na Mheza?

Supplementary Question 1

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mnamo mwezi Januari, 2008 Serikali ilituma wataalam kwenda kupima udongo katika vijiji hivyo vinne vya Mheza, Mpirani, Kadando na Maore; wananchi wanalipata matumaini makubwa sana, lakini mpaka sasa hivi hakuna kitu chochote kinachoendelea; nini kauli ya Serikali kwa wananchi hawa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; zao la mpunga ni zao la biashara ambalo wananchi wengi wanategemea katika maeneo hayo kwa ajili ya chakula pamoja na biashara ili kujikwamua kiuchumi.

Je, Serikali haioni umuhimu sasa wakufanya uharaka wa wa kuwajengea skimu hizo ili wananchi waweze kujikwamua kiuchumi? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, la kwanza; kazi kubwa ambayo tuliifanya kama Serikali ni kuhakikisha tunaipitia miradi yote ya umwagiliaji na kujua changamoto zake.

Mheshimiwa Spika, hatua ya pili ilikuwa ni kwenda katika utengaji wa fedha ili kuweza kutatua changamoto hizo. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba pamoja na huo mwaka alioutaja, lakini tumeielekeza Tume ya Taifa ya Umwagaliaji kwa ajili ya kwenda kufanya upembuzi yakinifu ili miradi hii ijengwe katika kiwango ambacho kitakuwa kinakidhi mahitaji na mwisho wa siku tusirudie kulekule tulipotoka kurekebisha skimu hizi mara kwa mara.

Kwa hiyo, nimuondoe hofu yakwamba kazi inaendelea kufanyika hivi sasa ni kutenga fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu ili tujenge mradi huu kwa ukamilifu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu uharakishaji wa jambo hili; na sisi tunafahamu ya kwamba moja kati ya mazao makubwa ambayo tunayategemea sana ni mazao ya mpunga kwa ajili ya chakula na hivyo tutahakikisha kwamba tunaharakisha zoezi hili ili wakulima wa maeneo hayo waweze kulima kwa wakati na mwisho wa siku tuisaidie nchi yetu ya Tanzania kupata chakula cha uhakika.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga skimu katika vijiji vya Maore, Mpirani, Kadando na Mheza?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi; zao la chai linahitaji sana umwagiliaji, ni lini Serikali italeta hizo scheme kwenye maeneo ya Igominyi, Tarafa ya Igominyi kwa ajili ya umwagiliaji wa chai?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, nimepokea swali la Mheshimiwa Mbunge, tutawaelekeza wenzetu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kuyapitia maeneo hayo ili kama kuna uwezekano na maeneo hayo yanaruhusu kuweka skimu hizo tuweze kuifanya kazi hiyo kwa uharaka.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga skimu katika vijiji vya Maore, Mpirani, Kadando na Mheza?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itajenga Skimu ya Mogahay, Dirimu na Yaeda Chini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hivi sasa tupo katika taratibu za kupitia skimu zote hizo kwa maana ya kuangalia status zake na hatua za kuchukua. Nimuahidi Mheshimiwa Mbunge ya kwamba pindi wataalamu wetu watakapopita na kuona hali ambayo imefikia tutaweka katika bajeti yetu ili tuweze kutekeleza mradi huo.

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga skimu katika vijiji vya Maore, Mpirani, Kadando na Mheza?

Supplementary Question 4

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, nini mkakati wa Serikali kuboresha na kuhimarisha umwagiliaji wa Agricultural Seed Agency (ASA) na hasa ikizingatiwa kwamba msimu wa kilimo uliopita wakulima walipata hasara kubwa kwani maji yalikuwa hayafiki kwenye mashamba yao?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika ni kweli tunayo mashamba kumi na saba yaliyo chini ya Wakala wa Mbegu Tanzania na hivi sasa baada ya kuongezewa bajeti katika eneo hili kutoka shilingi bilioni 10.5 mpaka shilingi bilioni 43 hivi sasa tunaweka mifumo ya umwagiliaji katika mashamba yetu na tumeanza katika Shamba la Nsimba pale Kilosa ambako tunajenga centre na lateral pivot kwa ajili ya kuhakikisha kwamba ASA anakuwa na uwezo wa kumwagilia mbegu katika mashamba yake mwaka mzima pasipo kutegemea mvua.