Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isitoe matibabu bure kwa watoto wenye ugonjwa wa selimundu?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, natambua kwamba watoto ambao wanazidi miaka mitano na wengi wao ni wale ambao wana Selimundu wamekuwa wakitozwa fedha katika hospitali ikiwemo hospital za Serikali.

Swali la kwanza, je, kwa kuwa hadi sasa Serikali inagharamia dawa za magonjwa kama UKIMWI, kifua kikuu na ukoma; kwa nini Serikali isiingize kwenye bajeti matibabu ya Selimundu kwa wagonjwa wa Selimundu ambao ni wachache kwenye bajeti ijayo kuanzia mwezi Julai?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa dawa zinazotibu Selimundu ikiwemo hii dawa inayoitwa hydroxyurea zimekuwa hazipatikani kwenye Wilaya nyingi ikiwemo Sikonge hali ambayo wagonjwa wanalazima kusafiri kwenda sehemu za mbali kama Mwanza au Dar es Salaam; kwa nini dawa hizi zisiletwe kwenye Wilaya ili zipatikane katika Wilaya kuondoa usumbufu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, labda nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia hili suala kwa ukaribu, lakini swali lake la kwanza kwamba ni kwa nini tusitenge bajeti?

Mheshimiwa Spika, Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan amefika mbali kwenye hili kwamba sasa kuna tiba ambayo inafanya gene editing kwa kutumia CRISPR-CAS9 technology ambayo ameshatafuta shilingi bilioni 11.5 kwa ajili ya kuanza, siyo tu kutibu kwa kupeleka dawa, lakini sasa kwenda kwenye genetic makeup ya mtu na kufanya diting ili kuweza kumtibu huyu mtu moja kwa moja na tiba hiyo siyo muda mrefu itaanza.

Mheshimiwa Spika, pia tutaona kwenye baadhi hospitali zetu za mikoa sasa zimeanza kutenga asilimia 10 ya bajeti yao mapato yao ya bima kuwasaidia watu hawa na ndiyo maana wakati wote tumekuwa tukiwasisitiza ninyi Wabunge tukikubaliana kwamba tutafika kwenye Bima ya Afya kwa Wote ni moja ya suluhisho hili la kutatua hili tatizo.

Hivyo Mheshimiwa Mbunge nakubaliana na wewe ni wazo zuri kutenga kwenye Bajeti.