Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 147 2023-02-10

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: -

Je, ni kwa nini Serikali isitoe matibabu bure kwa watoto wenye ugonjwa wa selimundu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge Sikonge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Matibabu ya watoto chini ya miaka mitano wenye matatizo ya kiafya ikiwemo Selimundu ni bure kwa mujibu wa Sera ya Afya ya mwaka 2007. Hivyo utambuzi na matibabu ya watoto wenye tatizo la selimundu hutolewa bila malipo.

Mheshimiwa Spika, suluhisho la tatizo hili ni Bima ya Afya kwa Wote.