Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi chenye hadhi ya Wilaya katika Jimbo la Singida Kaskazini?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru natambua juhudi hizo za Serikali, lakini kituo hicho cha polisi cha Kinyagigi ni kidogo, lakini pia kiko umbali mrefu kutoka yalipo majengo ya Serikali ikiwemo jengo la halmashauri, hospitali ya wilaya, benki pamoja na huduma za mahakama.

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kituo cha polisi chenye hadhi ya wilaya katika mji wa Ilongero?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kituo cha polisi kilichopo katika Mji wa Ilongero ni chakavu, hakina gari wala nyumba za watumishi. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuboresha huduma za kipolisi katika kituo hiki? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kituo cha polisi hadhi ya wilaya nadhani ni jambo la kuhitaji tafakuru na niko tayari kuzungumza na Mheshimiwa Mbunge kwa sababu tayari Wilaya ya Singida ina kituo cha ngazi ya wilaya, kinachotafutwa hapa ni kituo cha ngazi ya halmashauri. Sisi tunafahamu sote huwezi ukawa na OCD wawili ndani ya wilaya moja, lakini pale ambapo halmashauri ile itakuwa wilaya itakuwa rahisi ku- determine kwamba tunampeleka OCD and therefore anakuwa na ofisi yake, lakini tunatambua umuhimu wa kujenga kituo chenye hadhi kuliko hiki cha Daraja la C kwa sababu ni kituo kidogo.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge tutawasiliana kupitia Jeshi la Polisi tuone uwezekano wa kujenga kituo kikubwa kidogo kinachoweza kutekeleza majukumu zaidi ya kituo cha Daraja C.

Mheshimiwa Spika, kuhusu uchakavu tumesema tutaendelea kufanya ukarabati wa vituo vilivyo katika hali mbaya kutegemea uwepo wa fedha. Kwa mwaka huu nitaja juzi hapa baadhi ya vituo na kadri ya hali ya fedha itakavyoruhusu eneo hili la Ilongero litazingatiwa katika bajeti zetu, ahsante.