Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 146 2023-02-10

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi chenye hadhi ya Wilaya katika Jimbo la Singida Kaskazini?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abeid Ramadhani Ighondo Mbunge wa Singida Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kujenga vituo vya polisi katika maeneo mbalimbali nchini ili kuhudumia wananchi katika kudhibiti uhalifu. Katika tarafa ya Ilongero eneo la Kinyagigi Jimbo la Singida Kaskazini kunajengwa kituo cha Polisi cha Daraja C na kimefikia hatua ya umaliziaji. Kazi iliyobaki ni kuweka miundombinu ya umeme, maji safi na taka, milango na madirisha, dari, sakafu na kupaka rangi. Kiasi cha fedha shilingi 46,000,000 kinahitajika kumalizia ujenzi, na fedha hizo zinatarajia kutengwa kwenye bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2023/2024.