Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, ni nini mpango wa Serikali wa kupambana na majanga ya moto yanayotokea mara kwa mara kwenye masoko nchini?

Supplementary Question 1

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa matukio haya yamekuwa yanajitokeza mara kwa mara na inaonekana uwezo wa Wizara kupambana nayo bado ni mdogo.

Je, hawaoni umuhimu wa kurudisha huduma hii ya zimamoto kwa Halmashauri?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa sababu Mkoa kama wa Kilimanjaro una gari moja tu la zimamoto ambalo ni vigumu kuweza kufika mahali kwa muda mfupi. Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha angalau tunakuwa na gari la zimamoto kila Wilaya? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kuhusu kurejesha suala hili la zimamoto kwenye local governments, naomba nimkumbushe Mheshimiwa Mbunge kwamba lilikuwa hivyo kabla ya mwaka 2010 ikaonekana uwezo wa Serikali za Mitaa kumudu jukumu hilo ni mdogo sana na ikaelekezwa Serikali Kuu ichukue jukumu hilo na ndio sheria ikabadilishwa Serikali za Mitaa zikarejesha jukumu hilo ngazi ya kitaifa.

Mheshimiwa Spika, sasa tunachoweza kufanya ni kuimarisha na bahati nzuri kupitia bajeti ijayo tuna zaidi ya magari ya zimamoto 12 yatanunuliwa na uokozi yakiwemo magari yenye ngazi, lakini vilevile tumepata mkopo kutoka Austria ambao utasaidia kuimarisha uwezo wetu wa kupata vifaa kwa ajili ya kuzimia moto.

Kwa hiyo, tusikate tamaa tunaendelea kuimarisha jeshi hili bila shaka baadaye litaongeza weledi katika eneo hilo, nashukuru.

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, ni nini mpango wa Serikali wa kupambana na majanga ya moto yanayotokea mara kwa mara kwenye masoko nchini?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, barabara ya Tanzam ni muhimu sana na imekuwa magari ya mafuta yanawaka moto na Mkoa wa Songwe hatuna gari la zimamoto. Ni lini Serikali italeta gari ya zimamoto katika Mkoa wa Songwe?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itapatia Songwe; tumeweka kwenye bajeti katika magari 12 yatakayonunuliwa mwaka huu mikoa isiyokuwa na magari kabisa ikiwemo Songwe itapata gari hilo, ahsante.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, ni nini mpango wa Serikali wa kupambana na majanga ya moto yanayotokea mara kwa mara kwenye masoko nchini?

Supplementary Question 3

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, katika hayo magari yatakayokuja yananunuliwa na Serikali; je, Serikali iko tayari kupeleka gari moja katika Mji wa Ifakara?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwa sababu baadhi ya mikoa haina magari, siwezi kutoa ahadi hapa kwamba Ifakara watapata gari, lakini kadri tutakavyoongeza uwezo wetu wa kununua magari Wilaya zenye changamoto kubwa pia zitazingatiwa, nashukuru.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, ni nini mpango wa Serikali wa kupambana na majanga ya moto yanayotokea mara kwa mara kwenye masoko nchini?

Supplementary Question 4

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, kwenye hayo magari 12 ambayo Serikali imenunua; je, Wilaya ya Hai imo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwa sasa haimo, lakini mpango wa Serikali kadri utakavyoongeza uwezo wetu maeneo kama haya ambayo yamekuwa na usumbufu wa kuwaka moto msitu wetu unaozunguka Mlima Kilimanjaro kuwaka moto mara kwa mara yatazingatiwa katika bajeti zetu zijazo.

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, ni nini mpango wa Serikali wa kupambana na majanga ya moto yanayotokea mara kwa mara kwenye masoko nchini?

Supplementary Question 5

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa kuwa Sengerema ni sehemu ambayo ni ng’ambo ya Mwanza na tuna gari dogo sana ambalo lina uwezo wa kuchukua maji lita 500.

Je, Serikali iko tayari kutubadilishia tupate gari kubwa kwa sababu tuna-cover eneo kubwa mpaka Geita, ukichukua Buchosa na sasa hivi tuna mgodi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Sengerema inachukua eneo kubwa, lakini angalau wao wanalo gari moja japo dogo wengine hawana kabisa. Kwa hiyo, tutaendelea kuimarisha uwezo wetu ili baadaye Wilaya zote zikishapata then tutaingia uwezo wa kuongezea Wilaya ambazo zina magari madogo kama hayo.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, ni nini mpango wa Serikali wa kupambana na majanga ya moto yanayotokea mara kwa mara kwenye masoko nchini?

Supplementary Question 6

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, kwa nini Serikali isiweke kipaumbele ya kununua hayo magari ya zimamoto kwenye mikoa yote ambayo haina pamoja na Wilaya zote nchini?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nimejibu katika majibu ya swali la msingi kwamba katika bajeti ya mwaka huu tunaoendelea kutekeleza tutaanza kununua magari ambako mikoa isiyokuwa nayo itapewa kipaumbele baada ya hapo tutaingia kwenye Wilaya, nashukuru.