Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 145 2023-02-10

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: -

Je, ni nini mpango wa Serikali wa kupambana na majanga ya moto yanayotokea mara kwa mara kwenye masoko nchini?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Priscus Jacob Tarimo, Mbunge wa Moshi Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linaendelea na mikakati ya kuzuia majanga ya moto kwa kufanya ukaguzi wa masoko, kutoa ushauri wa kitaalam na utoaji wa elimu ya kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya moto. Jeshi pia linasisitiza kuwepo kwa vifaa vya awali vya kuzima moto (fire extinguishers) na ving’amuzi vya moto (fire detectors) na uwepo wa walinzi katika maeneo yote ya masoko.

Mheshimiwa Spika, napenda kuitumia fursa hii kuliarifu Bunge lako tukufu kwamba masoko yote nchini yamekaguliwa na wahusika kupewa ushauri stahiki. Jeshi pia linafanya ufuatiliaji ili kujiridhisha kama ushauri uliotolewa unafanyiwa kazi.