Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:- Mkoa wa Lindi umekuwa na shule chache za Kidato cha Tano na cha Sita, matokeo yake vijana wanaofaulu Kidato cha Nne kuingia Kidato cha Tano hupangiwa shule za mbali:- Je, ni kwa nini Serikali isifanye utaratibu wa kufanya Shule ya Sekondari Mchinga kuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi Kidato cha Kwanza hadi cha Sita?

Supplementary Question 1

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa shule hii ni siku nyingi sana imezungumzwa na Serikali kwamba itapandishwa hadhi kuwa shule ya Kidato cha Tano na Kidato cha Sita, lakini siyo kweli kwamba hii shule ina upungufu wa matundu ya vyoo, mimi shule hii naifahamu sana. Mwaka jana yamejengwa matundu 16, tatizo ni mabweni.
Swali langu la kwanza; je, Serikali ipo tayari hivi sasa kutenga bajeti ya kutosha ili shule hii ya Mchinga Sekondari waweze kujenga mabweni kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa Kidato cha Tano na cha Sita? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, amezungumza hapa Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba shule ya Kidato cha Tano na cha Sita, mwanafunzi kutoka Lindi na maeneo mengine anaweza kupangiwa mkoa wowote, lakini shule hizi za Kidato cha Tano na cha Sita Tanzania zina matatizo mengi ya chakula na wanafunzi wanakula milo ambayo siyo kamili, wanakula maharage ya kuoza maeneo mengi. Swali langu; Serikali iko tayari hivi sasa kuhakikisha kwamba inapeleka bajeti ya kutosha ili wanafunzi wa Kidato cha Tano na cha Sita Tanzania waweze kupata milo kamili?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza suala la kutenga fedha za kutosha, naomba nikiri kwamba katika mchakato wetu wa bajeti tulivyokuwa tunazungumza hapa, nilitaja miongoni mwa vipaumbele katika bajeti zetu. Vipaumbele vile viliji-reflect katika kila Halmashauri ilitenga nini. Tulikuwa na mpango mkakati mkubwa wa kuhudumia shule kongwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, jambo hili nadhani mchakato wake tulishaupitisha katika suala zima la mchakato wa bajeti. Halikadhalika Mkoa wa Lindi na vipaumbele vyake vimewekwa. Lengo kubwa ni nini? Kwa sababu ilikuwa ni maelekezo na Halmashauri ya Lindi ilishatenga baadhi ya fedha kwa ajili ya ku-facilitate hilo jambo. Lengo kubwa ni fedha zipatikane ziweze kupelekwa ilimradi kazi ile iweze kukamilika vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la kwamba shule hizi chakula chake, mgao wake hauendi vizuri; naomba niwaambie ndugu zangu, ni kwamba hili kama Serikali tumeliona na ndiyo maana kila wakati sasa hivi tunafanya rejea hata ya viwango vya posho ya kila siku ya chakula. Lengo letu ni kwamba, tufike muda tu-realize kwamba unit cost ya mwanafunzi kwa sasa ni kiasi gani, ili tunapokwenda katika mpango mpana kabisa wa kuhakikisha tunaboresha elimu Tanzania tuboreshe kwa ukubwa wake.
Naomba nikiri wazi kwamba Serikali inafanya kila liwezekanalo sasa hivi ili kutatua na kuongeza kiwango cha Walimu. Najua mpango huu mpana unapouanzisha ni lazima una changamoto yake kubwa. Sasa zile changamoto zinatupa sisi jinsi gani tutafanya tuweze kwenda vizuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana nimesema katika majibu yangu ya kwanza katika lile swali lake la kwanza la nyongeza kwamba ukiangalia sasa, zile shule kongwe tunaanza kuzibadilisha, tunakwenda kuziwekea miundombinu, lakini kuangalia ni jinsi gani watoto watakapokuwa katika mazingira ya shule waweze kupata elimu bora. Sambamba na hilo upatikanaji wa elimu bora unatokana na jinsi gani mtoto anapata lishe ya kutosha pale shuleni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Serikali inafanya utaratibu wote wa kina ili mwisho wa siku tuone elimu yetu Tanzania tunaipeleka wapi ilimradi tuweze ku-compete katika nchi nyingine za wenzetu za East Africa.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:- Mkoa wa Lindi umekuwa na shule chache za Kidato cha Tano na cha Sita, matokeo yake vijana wanaofaulu Kidato cha Nne kuingia Kidato cha Tano hupangiwa shule za mbali:- Je, ni kwa nini Serikali isifanye utaratibu wa kufanya Shule ya Sekondari Mchinga kuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi Kidato cha Kwanza hadi cha Sita?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Tatizo la shule hasa Kidato cha Tano na cha Sita ni la Kitaifa na hii inatokana na azma ya Serikali ya kuongeza Shule za Kata ambazo zilianzia Kidato cha Kwanza mpaka cha Nne. Nimeshangaa sana Naibu Waziri alipozugumzia kwamba hizi Shule za Kidato cha Tano na cha Sita ni za Kitaifa lakini hapo hapo anazungumzia habari ya Halmashauri kuendelea kujenga shule hizi. Je, anaweza akatuambia baada ya shule hizi za Kata, kuanzia Kidato cha Kwanza mpaka cha Nne, Serikali imeshajenga shule ngapi za Kidato cha Tano na cha Sita?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mwalimu Suzan Lyimo anafahamu, unapozungumzia Minaki, Tabora, Ilboru, Mzumbe zote ni Shule za Kitaifa hizo. Kwa hiyo, nilikuwa na maana kwamba huo ni msingi wa Shule za Kitaifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile tulielezea, kwa sababu tulikuwa na mchango mkubwa sana katika ujenzi wa shule za Kata na kila Halmashauri ilielekezwa kwa sababu watoto wengi watafaulu katika elimu ya Form Four, lakini idadi yetu ya shule zitakuwa ni chache kuwa-accommodate hao wanafunzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana kila Halmashauri imeelekezwa kufanya kila liwezekanalo miongoni mwa shule zao kubainisha miongoni mwa shule nyingine ziweze kuchukua advanced level, Form Five na Form Six. Hata hivyo, haikatazi, japokuwa wamekuza; mfano Shule ya Mchinga itakapokuwa Form Five na Form Six haitakataza mtoto kutoka Wanging‟ombe kwenda kule Mchinga, maana yake itakuwa ni room hiyo, watu kwenda maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ajenda yetu kubwa ni nini? Ni watu kupata elimu kadri iwezekanavyo. Amesema idadi ya takwimu, hata ukiangalia katika kanuni, nitampa takwimu, idadi halisi ya jinsi gani mchakato umekwenda. Sitaki kukupa jibu ambalo halitakuwa sawasawa hapa.