Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 27 Education, Science,Technology and Vocational Training, Ofisi ya Rais TAMISEMI. 220 2016-05-24

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:-
Mkoa wa Lindi umekuwa na shule chache za Kidato cha Tano na cha Sita, matokeo yake vijana wanaofaulu Kidato cha Nne kuingia Kidato cha Tano hupangiwa shule za mbali:-
Je, ni kwa nini Serikali isifanye utaratibu wa kufanya Shule ya Sekondari Mchinga kuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi Kidato cha Kwanza hadi cha Sita?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamidu Hassan Bobali, Mbunge wa Mchinga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na uhitaji mkubwa wa Shule za Sekondari Kidato cha Tano na Sita katika Wilaya ya Lindi, tayari Halmashauri ya Wilaya ya Lindi imependekeza Shule ya Sekondari ya Mchinga kuwa ya Kidato cha Tano na Sita. Hata hivyo shule hiyo ina upungufu ukosefu wa mabweni, matundu ya vyoo, jiko na bwalo la chakula. Halmashauri imeelekezwa kuweka vipaumbele na kutenga bajeti kwa ajili ya kurekebisha upungufu wa miundombinu ili shule hiyo iweze kupata sifa ya kusajiliwa na kuwa ya Kidato cha Tano na Sita.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya upungufu huo kurekebishwa na kukamilika, Serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, itatuma wataalam kwa ajili ya kukagua vigezo vilivyozingatiwa ili shule iweze kupandishwa hadhi kuwa ya Kidato cha Tano na Sita na endapo itaridhika itatoa kibali. Aidha, Shule za Sekondari za Kidato cha Tano na Sita ni za Kitaifa na kwa mantiki hiyo, zinapokea wanafunzi waliohitimu na kufaulu Mitihani ya Taifa ya Kidato cha Nne kutoka nchi nzima.