Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuwapatia wananchi wa Kyerwa Vitambulisho vya Taifa ili waondokane na adha wanayoipata?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa maelezo ambayo ameyaeleza Mheshimiwa Waziri inaonesha Ofisi ya NIDA imeshindwa kuwapatia Wanakyerwa vitambulisho, kwa sababu wananchi waliojitokeza ni 112,518. Wananchi waliopatiwa vitambulisho ni 31,897 ambayo ni asilimia 28. Kwa hiyo asilimia 71.7 bado hawajapatiwa vitambulisho.

Je, nani ambaye atalaumiwa kwa sababu wananchi hawa kutopatiwa vitambulisho hawawezi kusajili simu zao, wananchi hawa hawawezi kusajili hata kampuni, ni nani wa kulaumiwa katika hili?

Mheshimiwa Spika, swali lingine la pili kwa sababu inaonesha NIDA wameshindwa kutoa vitambulisho, kwa nini zoezi hili la NIDA lisisitishwe nchi nzima ili wakajipanga upya kuja kuwahudumia wananchi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Bilakwate kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja; wa kulaumiwa nani? Nadhani hilo tumeshapata suluhisho Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imeridhia kutoa fedha ambazo zilikwamisha kwa muda mrefu kutomlipa mzabuni zaidi ya bilioni 17. Baada ya kumlipa mzabuni mkataba umehuishwa na uzalishaji wa vitambulisho unaendelea. Na tuishukuru Wizara ya Fedha imeanza kutoa katika bajeti fedha iliyopitishwa katika bajeti bilioni 42 imeshatoa zaidi ya bilioni 10 ili kumlipa mkandarasi aanze kuzalisha vitambulisho hivyo. Kwa mwenendo huu nina uhakika wananchi wote watapata vitambulisho kama ilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Spika, ili suala la kwamba wameshindwa sasa tusitishe; sasa tuko kwenye mkataba na Serikali imeshaji- commit kutoa fedha sasa unasitisha ili u-achieve nini wakati vitambulisho bado ni muhimu. Jambo la msingi watekelezaji wetu wa Serikali maeneo mbalimbali kama mtu ana namba ya utambulisho tumeshatoa mwongozo kwamba namba ile itumike kama kitambulisho, kama kuna mahali mtu anakwamisha tupeane taarifa ili hatua ziweze kuchukuliwa, nashukuru.