Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 144 2023-02-10

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuwapatia wananchi wa Kyerwa Vitambulisho vya Taifa ili waondokane na adha wanayoipata?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Jimbo la Kyerwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Januari, 2023 jumla ya wananchi 112,518 wamesajiliwa na kutambuliwa Wilayani Kyerwa. Vilevile katika kipindi hicho jumla ya Namba za Utambulisho (National Identification Numbers) 31,897 sawa na asilimia 28.3 ya wananchi wote walioandikishwa zimezalishwa na kugawiwa kwa wananchi wa Wilaya hiyo. Aidha, jumla ya Vitambulisho vya Taifa 19,614 sawa na asilimia 61.5 ya Namba za Utambulisho vimezalishwa na kugawiwa kwa wananchi wa Wilaya ya Kyerwa.

Mheshimiwa Spika, mkakati unaotekelezwa na Serikali ni kusimamia kwa karibu mkataba uliohuishwa ili fedha shilingi bilioni 42.5 zilizotengwa zikitolewa na kulipwa mzabuni azalishe na kuwasilisha kadighafi 13,000,000 ili uzalishaji wa Vitambulisho vya Taifa uendelee kutekelezwa. Ununuzi wa kadighafi hizo utawezesha mamlaka kuzalisha vitambulisho kwa wananchi wote waliosajiliwa na kutambuliwa ikiwemo wananchi wa Wilaya ya Kyerwa, ahsante.