Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tamima Haji Abass

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TAMIMA HAJI ABASS aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kutoa elimu kwa jamii dhidi ya udhalilishaji na ukatili wa watoto?

Supplementary Question 1

MHE. TAMIMA HAJI ABASS: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; je, Serikali imefanya utafiti na tathmini na kujua kama elimu inayotolewa inatija na inaleta mabadiliko katika jamii? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Serikali haioni haja sasa kutumia taasisi za dini kuiandalia programu maalum kwa ajili ya kutoa elimu kusaidia kukinga vitendo hivyo? (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Tamima, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza; kupitia MTAKUWA uliomaliza muda wake 2020/2021 uliotolewa kwenye Kikao cha Mawaziri wa Wizara mtambuka kilichofanyika tarehe 26 Januari, 2023 inaonesha kuwa jamii iliyopewa elimu inapata tija kwa jamii na inaendelea kuripoti taarifa za vitendo vya ukatili katika vyombo vya usalama.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, Serikali kwa kushirikiana na madhehebu ya dini nchini itaendelea kutekeleza programu ya malezi kwa ajili ya kutoa elimu ya kujikinga na vitendo vya ukatili katika taasisi zote za dini, ahsante.

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. TAMIMA HAJI ABASS aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kutoa elimu kwa jamii dhidi ya udhalilishaji na ukatili wa watoto?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Je, Serikali haioni iko ya haja ya udhalilishaji na ukatili wa wanawake na watoto kuwa ajenda ya kitaifa? (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maryam, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Maryam, ushauri wake tumeupokea na tutaufanyia kazi kwa sababu vitendo vya ukatili ni vya jamii na jamii yote tunatakiwa tushirikiane kwa pamoja ili kuungana na kupinga vitendo vya ukatili nchini, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TAMIMA HAJI ABASS aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kutoa elimu kwa jamii dhidi ya udhalilishaji na ukatili wa watoto?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; niulize hivi, je, Serikali haioni haja sasa ya kutoa tamko la kuondoa udhalilishaji wa watoto wa kike wanaoolewa chini ya miaka 18 badala ya kusubiri maoni ya wadau kwa kitu ambacho kiko wazi? (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, napenda kutoa jibu kwa Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ina taratibu zake na mtoto wa kike anaruhusiwa kuwa na umiliki wa kitu cha peke yake kuanzia miaka 18. Kwa hiyo, ushauri huo tunaomba tuendelee na kuwapa Serikali majukumu haya ili kuhakikisha nini tunakifanya katika nchi yetu, ahsante. (Makofi)

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TAMIMA HAJI ABASS aliuliza: - Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kutoa elimu kwa jamii dhidi ya udhalilishaji na ukatili wa watoto?

Supplementary Question 4

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi.

Moja ya vichocheo vikubwa vya udhalilishaji wa wanawake na watoto ni picha za ngono zilizoko katika mitandao, nchi za Uarabuni zimefanikiwa kuzuia kitu wanachoita Uniform Resource Locators (URL) ili picha za ngono zisionekane katika nchi ile.

Je, Serikali haichukui hatua sasa kuzuia picha za ngono kuonekana katika mitandao yetu ya simu ili kuokoa vijana wetu?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abbas kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutoa elimu kwa ajili ya kujikinga na vitendo vya ukatili kwa watoto wote kupitia vijarida mbalimbali na pia Serikali inakataza kutoa picha za ngono katika mitandao. Mtu yeyote ambaye atafanya vitendo hivyo na akagundulika, basi hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake. (Makofi)

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA
HABARI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niongezee maelezo kidogo kwenye swali lililoulizwa na Ndugu Tarimba Abbas, Mbunge wa Kinondoni.

Mheshimiwa Spika, katika maendeleo ya TEHAMA, moja ya changamoto kubwa tunayoipata ni udhibiti huo wa baadhi ya taarifa ambazo kwa kweli zinamomonyoa utamaduni na maadili ya nchi yetu, lakini kupitia TCRA tumeongeza uwekezaji mkubwa na sasa tuko katika hatua za mwisho za kuongeza nguvu ya kudhibiti movement ya picha kama hizo kwa kuweka gateways. Uwekezaji huu ukikamilika na ufungaji wa mifumo hii ukikamilika, hili jambo tutakuwa tumelidhibiti kwa kiwango kikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilithibitishie Bunge lako, tunao uwezo mpaka sasa wa kufuatilia na kujua nani anasambaza picha chafu. (Makofi)

Kwa hiyo, nitoe tahadhari kwa watu ambao wanatumiwa picha, njia rahisi ukitumiwa picha chafu usimtumie mtu, ni bora ukaifuata kwa sababu ukimtumia mtu mamlaka zina uwezo wa kujua nani kamtumia nani.