Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, Serikali imechukua hatua gani ili kumaliza mgogoro uliopo kati ya Mbuga ya Rwanyabara na Kijiji cha Bushasha kata ya Kishanje Wilayani Bukoba ambao umedumu kwa muda mrefu?

Supplementary Question 1

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri, lakini mimi nina swali moja tu la nyongeza, linaweza kuchukua muda kidogo, naomba unilinde.

Mheshimiwa Spika, mgogoro huu upo kati ya mwanakijiji na wanakijiji na umechukua muda mrefu zaidi ya miaka 15 na mgogoro huu unafahamika katika Serikali ya Kata, Serikali ya Wilaya, Serikali ya Mkoa na wameshindwa kufanya suluhu yeyote.

Kwa hiyo, sasa nomba Serikali sasa ione muda muafaka kwa Wizara ambayo wanaona inahusika na swali hili, wafike katika kijiji hicho, wafanye suluhu ili huyu mwanakijiji apate haki yake na wanakijiji wapate haki yao, ahsante. (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mhesimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Conchesta, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niziombe tu Serikali zilizoko kwenye Mamlaka ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa wakishirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi washughulikie mgogoro huu ili sasa wananchi waweze kupata haki yao na huyo mwekezaji aliyeko katika maeneo hayo pia aweze kufanyiwa haki yake, ahsante. (Makofi)

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, Serikali imechukua hatua gani ili kumaliza mgogoro uliopo kati ya Mbuga ya Rwanyabara na Kijiji cha Bushasha kata ya Kishanje Wilayani Bukoba ambao umedumu kwa muda mrefu?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini Serikali itashughulikia migogoro ya wafugaji na wakulima inayoendelea katika maeneo yanayozunguka Hifadhi ya Serengeti? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Agnes Marwa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kumekuwa na changamoto kubwa katika Hifadhi ya Serengeti na wananchi ama vijiji vinavyozunguka hifadhi hiyo na changamoto hizi zimesababisha kuwepo na vurugu nyingi ikiwemo wananchi kuuawa lakini pia na askari wameendelea kuuawa.

Mheshimiwa Spika, tayari Serikali imeshaanza kuchukua hatua na kama siku tatu zilizopita Serikali ya Mkoa ilienda kuzungumza na wananchi ili kutatua mgogoro huu. Kimsingi hakuna mgogoro wowote isipokuwa wananchi hawataki kukubaliana na mipaka iliyopo na kibaya zaidi tunapoweka vigingi wananchi wanaenda wanang’oa vile vigingi na kuendelea kufanya vurugu ikiwemo kuingiza mifugo hifadhini.

Kwa hiyo, niendelee kuwaomba wananchi wafuate sheria na taratibu zilizopo nchini, kwenda kinyume na sheria ni kujitakia sababu nyingine ambazo Serikali itachukua hatua.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Naibu Waziri namshukuru sana, lakini naomba nitumie nafasi hii kusema kwamba eneo la Serengeti ni miongoni mwa maeneo ya vivutio vyetu ambavyo vinajulikana kimataifa. Hili ni eneo ambalo tunapaswa kulilinda na kuliendeleza, lakini hili ni eneo pia ambao kumekuwa na changamoto kama alivyosema Naibu Waziri, askari wetu mara kwa mara wamekuwa wakipigwa mishale na wananchi wanaozunguka.

Mheshimiwa Spika, wiki iliyopita Askari Deus mwenye umri wa miaka 42 amepigwa mshale wa sumu eneo lile na tumekuwa tukiendelea wananchi na kutoa matamko na kulaani hali hii.

Mheshimiwa Spika, hivyo nitumie nafasi hii kusema kwamba kimsingi Serengeti haina mgogoro wowote wa mpaka, wananchi wanapaswa kufahamu na niishukuru sana Kamati ya Ulinzi na Usalama ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara wamepita juzi na wataalam wetu, kuwaonesha wananchi eneo la mpaka ili wasipate kuingia katika hifadhi.

Hivyo ni muhimu kuheshimu maeneo haya ya hifadhi ili hifadhi zetu ziwe salama, wafugaji wawe salama na wakulima wawe salama. Nimeona niongeze msisitizo huo, nashukuru sana. (Makofi)