Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 139 2023-02-10

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: -

Je, Serikali imechukua hatua gani ili kumaliza mgogoro uliopo kati ya Mbuga ya Rwanyabara na Kijiji cha Bushasha kata ya Kishanje Wilayani Bukoba ambao umedumu kwa muda mrefu?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kijiji cha Bushasha kipo Kata ya Kishanje katika Wilaya ya Bukoba. Kijiji husika hakipakani na hifadhi yoyote ya wanyamapori katika Mkoa wa Kagera. Aidha, hakuna mgogoro wowote kati ya Kijiji cha Bushasha na hifadhi yoyote ya wanyamapori zilizopo katika Mkoa wa Kagera.

Mheshimiwa Spika, mgogoro uliokuwepo katika Wilaya ya Bukoba ulikuwa kati ya Kijiji cha Kangabusharo katika Vitongoji vya Nshisha, Kangabusharo na Kayaga na Hifadhi ya Msitu wa Ruasina ambao tayari umefanyiwa kazi na timu ya wataalam.