Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA Wilayani Serengeti ili vijana wanaomaliza elimu ya msingi na sekondari wapate ujuzi?

Supplementary Question 1

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, awali ya yote ninaishukuru sana Serikali na kipekee kabisa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia kwa kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa VETA Wilayani Serengeti.

Mheshimiwa Spika, watu wa Serengeti wamekuwa na uhitaji wa chuo hiki kwa muda mrefu sana jambo ambalo lilipelekea kumfuata mara kwa mara Waziri, Naibu Waziri kuwataka kutusaidia kupata fedha kwa ajili ya ujenzi wa chuo hiki.

Sasa niiombe Serikali itoe kauli ya ni lini chuo hiki wataanza ujenzi wake pamoja na maandalizi yote yanayoendelea, lakini tunataka kujua ni lini ujenzi utaanza? Hilo ni swalila kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kutokana na changamoto za kijiografia pamoja na mahitaji maalumu ya Serengeti, niliiandikia Wizara proposal ndogo ya kuboresha kile chuo ambacho watajenga Serengeti.

Sasa je, Waziri au Naibu Waziri pamoja na wataalam wake wapo tayari kuja Serengeti kuona mazingira na kufanya need assessment kwa sababu proposal hii itahitaji nyongeza ya fedha kidogo na hivyo watapata uelewa mpana na kutusaidia katika proposal hii? Ahsante sana.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jeremiah Mrimi, Mbunge wa Serengeti kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri ni kweli Mheshimiwa Mbunge toka mwaka 2021 amekuwa akifika ofisini mara kwa mara, lakini hata hapa Bungeni tukionana mara kwa mara alikuwa akinikumbusha jambo hili, lakini mara kadhaa nadhani amefika kwa Mheshimiwa Waziri pamoja na kupiga simu kufuatilia jambo hili.

Kwanza nikushukuru Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji huo wa karibu kwa kuwafuatilia wananchi wa Serengeti tunakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, kipekee nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, siyo kwa kutenga tu fedha.

Mheshimiwa Spika, naomba nikuhakikishie kwamba hii shilingi bilioni 100 tayari Mheshimiwa Rais ameshaitoa, kwa hiyo, ni jukumu letu sisi kama Wizara sasa kusimamia kwa karibu.

Kwa hiyo, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge hivi sasa tuko kwenye maandalizi, hauwezi ukasema tu kwamba utaanza kesho kwa sababu kuna taratibu ambazo lazima tuzifanye. Nimesema hapa maeneo tayari tumeshapata, tumebainisha maeneo yale na hivi sasa tunafanya topographical survey, lakini vilevile lazima tufanye geo-technical survey, lakini vilevile lazima tufanye environment impact assessment ili wakati tunapoanza tusiweze tena kupata changamoto.

Kwa hiyo, nikuhakikishie tu kwamba taratibu hizi zitakapo kamilika ujenzi huu utaanza mara moja.

Mheshimiwa Spika, katika eneo la pili, kwa upande wa kuja sisi aidha mimi au Waziri na wataalam, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge tupo tayari kwenda Serengeti ili kuweza kuona changamoto na namna gani tunaweza kuzifanyia kazi, nashukuru sana.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA Wilayani Serengeti ili vijana wanaomaliza elimu ya msingi na sekondari wapate ujuzi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, nimesikiliza majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusiana na Wilaya 63 ambazo mnatarajia kujenga VETA katika mwaka huu wa fedha.

Je, Wilaya ya Kigamboni ni moja ya Wilaya hizo unaweza ukalithibitisha hilo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Kigamboni, kaka yangu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimuondoe hofu Mheshimiwa Dkt. Ndugulile kwamba katika orodha na mimi nimeipitia vizuri na Wilaya ya Kigamboni ni miongoni mwa Wilaya ambazo ziko kwenye mpango wa kujengewa vyuo hivi na bahati nzuri maeneo yameshatengwa kwa ajili ya ujenzi na mimi Mheshimiwa Mbunge baada ya Bunge hili kwa vile niko karibu pale tutakwenda kulitembelea na kuona namna hani tunaweza tukafanya. (Makofi)