Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 9 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 137 2023-02-10

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA Wilayani Serengeti ili vijana wanaomaliza elimu ya msingi na sekondari wapate ujuzi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jeremiah Mrimi Amsabi, Mbunge wa Jimbo la Serengeti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni azma ya Serikali kujenga Chuo cha Ufundi Stadi katika kila Mkoa na Wilaya nchini. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa vyuo vya VETA katika Wilaya 63 ambazo hazina vyuo hivyo. Kiasi hiki pia kitatumika katika ujenzi wa chuo cha VETA cha Mkoa wa Songwe. Serengeti ni miongoni mwa Wilaya 63 ambazo zipo kwenye mpango wa kujengewa Vyuo vya Ufundi Stadi katika mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali imeshakamilisha maandalizi ya awali ikiwemo upatikanaji wa maeneo kwa ajili ya ujenzi pamoja na kuandaa michoro na makadirio ya gharama za ujenzi kwa kila chuo na ujenzi huo unatarajiwa kuanza mara tu taratibu za manunuzi zitakapokamilika, nashukuru sana.