Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutoa chakula cha bei nafuu kwa wananchi wa Jimbo la Arumeru Magharibi kutokana na athari za ukame?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Arumeru hususan Kata 13 ambayo ndio imekubwa na njaa imepakana na Longido, Ngorongoro na Monduli. Katika Wilaya hizo za Ngorongoro, Monduli na Longido chakula kimeuzwa shilingi 700 kwa wananchi, lakini katika upande wa Arumeru Magharibu chakula wananchi wanaambiwa wanauziwa shilingi 885.

Je, ni kwa nini bei katika Wilaya zingine ni shilingi 700 na Arumeru Magharibi ni shilingi 885 na wakati tuko sehemu moja na hali ni hiyo hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa kuna hilo tatizo Waziri haoni haja ya kufika katika Jimbo la Arumeru Magharibi au Wilaya ya Arumeru ili aweze kuona hali halisi ilivyo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu, Mbunge wa Arumeru Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jambo ambalo Mheshimiwa Mbunge ameliuliza hapa tulishawasiliana naye na tulitoa ufafanuzi ambao nataka niurudie hapa.

Mheshimiwa Spika, hoja ya kwanza ya Mheshimiwa Mbunge ni juu ya kituo kuwepo katika eneo ambalo haligusi katika jimbo lake na hivyo wananchi katika eneo lake wanachukua umbali mrefu na bei imekuwa ikiongezeka sana kuweza kupata ile bei ambayo maeneo mengine wanapata.

Mheshimiwa Spika, nilishasema hapa Bungeni ya kwamba katika mazao haya ya mahindi ya bei nafuu, chakula cha bei nafuu kama Mheshimiwa Waziri alivyosema tunapeleke kwenye Halmashauri ya Wilaya na vituo ndiyo vinatengenezwa hapo, lakini ikitokea kwamba katika baadhi ya maeneo kuna umbali mrefu, NFRA tumeshawapa maelekezo ya kusogeza vituo hivyo ili kuweza kuwahudumia watu wote kwa ukaribu zaidi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo katika maelezo ya awali kama katika eneo lake alikuguswa mimi nitatoa maelekezo siku ya leo kuhakikisha kwamba NFRA wanaongeza vituo ili na jimboni kwake pia paweze kuguswa na iweze kupunguza pia hali ya bei kwa sababu moja kati ya changamoto kubwa inayosababisha pia ni kwa sababu ya umbali ambao wamekuwa wakiupiga NFRA.

Kwa hiyo, kwa ujumla wake tumwachie Mheshimiwa Mbunge ya kwamba tutahakikisha pia katika uongezaji wa vituo tutagusa na jimbo lake ili wananchi wake wasiende umbali mrefu na bei pia isiweze kuwa kubwa kama ilivyo hivi sasa. (Makofi)

SPIKA: Ameuliza kuhusu kwenda kujiridhisha.

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kuhusu kwenda kujiridhisha hiyo ni kazi yangu mimi kama Naibu Waziri, nilitaka nimhakikishie kwamba nipo tayari baada ya Bunge hili nitakwenda katika eneo hilo kwenda kujiridhisha katika hali ambayo ameisema. (Makofi)

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutoa chakula cha bei nafuu kwa wananchi wa Jimbo la Arumeru Magharibi kutokana na athari za ukame?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa Serikali imetuletea mahindi kwenye vituo viwili kwa maana ya Segese na Isaka na kuacha kata zingine 16 ambazo ziko umbali mrefu kutoka kwenye kata zile.

Mheshimiwa Spika, ahsante. Ni lini Serikali itawatuma NFRA kuja kuongeza idadi ya vituo kwenye kata ambazo ziko mbali na maeneo hayo husika?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim, Mbunge wa Msalala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa chakula cha bei nafuu Halmashauri husika huwa wanatuambia eneo ambalo limeteuliwa, lakini kutokana na changamoto za wananchi wetu wanatoka maeneo ya mbali tumeishatoa maelekezo kwa NFRA kuhakikisha kwamba wanaongeza vituo zaidi ili wananchi wengi waweze kuhudumiwa kwa ukaribu. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba katika Jimbo la Msalala tutazingatia pia hiyo ili wananchi wake wasitembee umbali mrefu kufuata chakula hiki cha bei nafuu.

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutoa chakula cha bei nafuu kwa wananchi wa Jimbo la Arumeru Magharibi kutokana na athari za ukame?

Supplementary Question 3

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Halmashauri ya Mji wa Bunda kuna wananchi wanaishi zaidi ya kilometa 40 kuja Kata ya Bunda Store ambapo ndipo kituo cha kuuzia mahindi kilipo.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kituo kingine cha usambazaji mahindi? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Chacha Maboto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kwamba kutokana na mahitaji hayo nitatoa maelekezo kwa Wakala wa Hifadhi ya Chakula kuhakikisha wanaongeza kituo kingine zaidi ili wananchi wasitembee umbali mrefu.