Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - (a) Je, ni kwa nini Serikali isiongeze uzalishaji wa mafuta ya alizeti nchini kwa ajili ya Soko la Zanzibar na Bara kuliko kuagiza kutoka nje ya nchi? (b) Je, hali ya uzalishaji wa mafuta ya alizeti ikoje kwa mwaka na ni mikoa gani inayozalisha zaidi Tanzania Bara?

Supplementary Question 1

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, ningependa kujua kwa vile kuna taasisi ya ASA ambayo Serikali iliipa dhamana ya kutoa mbegu katika msimu wa mwaka 2020/2021; zile mbegu hazikufanya vizuri na wakulima wengi ambao wamezitumia zile mbegu wamepata hasara.

Je, nini kauli Serikali katika kuwafidia wale wakulima ambao wamekula hasara kutokana mbegu zile za taasisi ya ASA? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Serikali mmejipangaje sasa kuhakikisha haitokei tena wakulima wadogo wadogo ambao wanapata mbegu kutoka taasisi ile ya ASA wakaingia tena hasara ili wakaendelea kuwa maskini zaidi? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbuni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika msimu alioutaja Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) alisambaza mbegu za alizeti ambazo katika baadhi ya maeneo zilifanya vizuri na pia katika baadhi ya maeneo hazikufanya vizuri.

Mheshimiwa Spika, ziko sababu nyingi zilizopelekea kutokufanya vizuri hasa kutokana na misimu ya kupanda na changamoto zingine zilizosababishwa na mabadiliko ya tabianchi. Iko mikoa ambako mbegu hizi zilistawi vizuri na wananchi wamevuna, wamepata mavuno makubwa na tumekuwa tukichukua kama sehemu ya kielelezo.

Mheshimiwa Spika, katika kuitatua changamoto hii katika mwaka huu wa fedha wa 2022/2023 Serikali imetenga fedha kuhakikisha kwamba tunazalisha mbegu, tunazigawa kwa ruzuku kwa wakulima ambazo ni certified seed tofauti na zile ambazo zimewekwa awali na lengo letu ni kuhakikisha kwamba wakulima wazipate mbegu hizi kwa bei rahisi ya ruzuku kwa kilo mbili kwa shilingi 10,000 ili ziweze kuwasaidia kutokana na changamoto ambayo waliipata.

Mheshimiwa Spika, vilevile tumehakikisha kuanzia hivi sasa tumempa maelekezo ASA tutaanza kuzalisha certified seeds ili wakulima wetu waweze kulima na waweze kupata tija kutokana na kilimo cha alizeti.

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - (a) Je, ni kwa nini Serikali isiongeze uzalishaji wa mafuta ya alizeti nchini kwa ajili ya Soko la Zanzibar na Bara kuliko kuagiza kutoka nje ya nchi? (b) Je, hali ya uzalishaji wa mafuta ya alizeti ikoje kwa mwaka na ni mikoa gani inayozalisha zaidi Tanzania Bara?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, nilitaka kufahamu ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuimarisha soko la zao la vanila mkoani Kagera? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Neema Lugangira, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli zao la vanila hivi sasa limeanza kupata muamko mkubwa na wakulima wengi wamehamasika kulima zao hili na sisi kama Serikali tumeendelea kufatilia hatua kwa hatua kuhakikisha kwamba tunaweka mazingira bora na wezeshi kuwafanya wakulima wetu waweze kunufaika na zao hili.

Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba ni sehemu pia ya mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba tunatengeneza miundombinu rafiki na mazingira rafiki ili wakulima wetu waweze kunufaika na uzalishaji wa zao la vanila.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - (a) Je, ni kwa nini Serikali isiongeze uzalishaji wa mafuta ya alizeti nchini kwa ajili ya Soko la Zanzibar na Bara kuliko kuagiza kutoka nje ya nchi? (b) Je, hali ya uzalishaji wa mafuta ya alizeti ikoje kwa mwaka na ni mikoa gani inayozalisha zaidi Tanzania Bara?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, siku za karibuni kupitia vyombo vya habari tumeshuhudia mama mmoja ambaye alifika Zanzibar akiwa na ndizi na alipigwa faini, akatakiwa arudi na bidhaa hiyo upande wa Bara. Lakini wote tunaelewa kwamba Tanzania ni nchi moja.

Ni nini kinasababisha kwamba bidhaa kama hizo zikienda upande wa pili zinarudishwa na nini kauli ya Serikali kwenye hili?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nishukuru kwa busara yako njema ya kuongoza Bunge letu hili tukufu.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Dada Paresso alizungumza suala zima la kuzuiliwa kwa ndizi za mama mmoja wiki iliyopita ambapo Watanzania walishuhudia jambo lile likitokea katika mitandao ya kijamii. Na kweli mimi mara baada ya kuona jambo lile kwa sababu ninahusika na dhamana ya Muungano wetu, lakini nikifahamu kwamba Muungano wetu katika mambo tunafanya vizuri katika upande wa Muungano maeneo yote mawili. Ililazimu ofisi yangu kwa haraka sana kuwasiliana na ofisi ya mwenzangu, Mheshimiwa Hamza, Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili Zanzibar, kumuuliza kulikoni ninachokiona katika mitandao?

Mheshimiwa Spika, Waziri mwenzangu alinijibu ya kwamba jambo hilo ni kweli limetokea, lakini ni kwa sababu kufuatia Tangazo la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambalo limetolewa kwa mujibu wa Sheria Namba 9 ya mwaka 1997, Sheria ya Uhifadhi wa Mimea, na tangazo hilo limetokana na hivi karibuni imebainika kuna ugonjwa wa mnyauko wa migomba ambao unaitwa Banana Xanthomonas Campestris.

Mheshimiwa Spika, kutokana na hilo sasa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliamua kutoa tangazo maalum la kuzuia mazao yote ya migomba ikiwemo ndizi, mimea na majani kwa lengo la kuepusha ugonjwa huo usisambae katika maeneo mbalimbali, lakini wakatoa maelekezo katika maeneo yote ya kuingilia vyombo mbalimbali kuzuia mimea hiyo isiweze kuingia.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa mujibu wa Sheria hiyo Namba 9 ya mwaka 1997; endapo kosa hilo litabainika kuna adhabu zake tatu, jambo la kwanza aliyehusika kuingiza mimea hiyo anapaswa kuiteketeza kwa gharama zake mwenyewe; ahabu ya pili ni kwamba anaweza akapewa fine ya 50,000 kulipa ama zaidi ya hapo na adhabu ya tatu, anaweza akaelekezwa ya kwamba adhabu yake ni kifungo cha miezi sita kwenda gerezani miezi sita ama adhabu zile mbili kwa pamoja. Hii ni kwa mujibu wa Sheria Namba 9 ya mwaka 1997.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tangazo hili lilikuwa limetoka na kuwekwa katika maeneo yote ya kuingilia kwa mipaka ile. Tunafahamu kwamba kila nchi duniani ina utaratibu au kila maeneo mamlaka zina taratibu zake za kulinda.

Kwa hiyo, hili lilikuwa ni suala zima la udhibiti, lakini kwa bahati mbaya mama yule alikuwa hafahamu kwamba kuna lile tangazo lilitoka kabla. Kwa hiyo, ndio maana tulipofuatilia tulipata majibu hayo kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na ni kweli tangazo lile lilitoka kwa kuziia suala zima la ugonjwa wa mnyauko wa migomba usiingie katika upande wa Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, sisi katika hilo tukaona basi ni vyema tangazo lile likatolewa kwa uwazi zaidi. Lengo kubwa ni kwamba watu wasiofahamu kwamba kuna zuio la kuingiza mazao ya migomba basi kila Mtanzania aweze kulipata kwa ajili ya kuchukua tahadhari hizo.

Mheshimiwa Spika, na hicho ndicho kilichojiri kule Zanzibar. Kwa hiyo, mpaka hivi sasa tangazo lile ni tangazo halali la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, limewekwa kwa ajili ya kuzuwia mimea hasa mazao ya migomba, ndizi zake, migomba na majani yasiingie kwa ajili ya kuzuia suala zima la uambukizaji wa ugonjwa wa mimea hii ya ndizi.

Mheshimiwa Spika, huu ndio mustakabali wa jambo hili. Kwa hiyo, hili wenzetu wameli-treat hivyo, lakini ni kwa mujibu wa Sheria ya Quarantine kule utaratibu wa kuhifadhi mimea katika eneo hilo. Naomba kuwasilisha. (Makofi)