Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 8 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 129 2023-02-09

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: -

(a) Je, ni kwa nini Serikali isiongeze uzalishaji wa mafuta ya alizeti nchini kwa ajili ya Soko la Zanzibar na Bara kuliko kuagiza kutoka nje ya nchi?

(b) Je, hali ya uzalishaji wa mafuta ya alizeti ikoje kwa mwaka na ni mikoa gani inayozalisha zaidi Tanzania Bara?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbuni lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mkakati wa kuongeza uzalishaji wa mazao ya mafuta nchini kwa lengo la kupunguza uagizaji wa mafuta ya kula na kuongeza uzalishaji kutoka wastani wa tani 700,000 hadi tani 1,500,000 ifikapo mwaka 2025. Utekelezaji wa mpango huo unajumuisha ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji kwenye mashamba ya mbegu ya Wakala wa Mbegu za Kilimo ambapo kwa mwaka 2022/2023 jumla ya shilingi bilioni 43.03 zitatumika kwa lengo hilo.

Mheshimiwa Spika, mahitaji ya mafuta ya kula nchini ni tani 650,000 kwa mwaka. Tathmini ya mwaka 2020/2021 inaonesha kuwa uzalishaji wa ndani wa mafuta ya alizeti ni asilimia 75 ya kiasi cha wastani wa tani 300,000 za mafuta ya kula yanayozalishwa nchini kwa mwaka. Mikoa inayozalisha alizeti kwa wingi ni Singida, Dodoma, Manyara, Shinyanga, Iringa, Tabora, Morogoro, Ruvuma, Mbeya, Arusha, Lindi, Mtwara, Rukwa na Mara.