Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga mradi mpya wa maji safi na salama kuliko kuendelea na ukarabati wa Mradi wa Kata ya Kihurio ambao ulijengwa mwaka 1967?

Supplementary Question 1

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nikiri kwamba nimelipenda sana jibu la Serikali, lakini zaidi ya hapo naomba niulize swali moja tu la nyongeza.

Kwa kuwa ni miaka 55 iliyopita tangu mradi huu ambao tunautumia sasa ulipojengwa na kwa kuwa walipoujenga mradi huu, chanzo cha maji kilikuwa kimoja kwa sababu Kata ya Kihurio ilikuwa na vijiji viwili tu na kwa kuwa sasa hivi Kata ya Kihurio ina vijiji vitano na population imekuwa kubwa sana takribani watu zaidi ya 10,000.

Je, Serikali haioni kwamba itakapojenga mradi huu mpya, ijenge vyanzo vya maji ambavyo ni zaidi ya chanzo kimoja?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anne Kilango kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru kwa kuridhika na majibu ya Serikali, lakini vilevile nikupongeze kwa ufuatiliaji wa eneo hili la Kihurio.

Mheshimiwa Spika, sisi kama Wizara kila ongezeko linapotokea la watumia maji, tunaboresha vyanzo na intake zetu hivyo Mheshimiwa Mbunge hili nimelipokea na tutalizingatia wakati tunatekeleza mradi huu mkubwa.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga mradi mpya wa maji safi na salama kuliko kuendelea na ukarabati wa Mradi wa Kata ya Kihurio ambao ulijengwa mwaka 1967?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Kwanza niishukuru Serikali kwa kuchimba maji katika Mradi wa Dambia na yanapatikana kwa wingi.

Je, Mheshimiwa Waziri lini mnajenga Mradi ule wa Dambia ambao unaufahamu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Massay kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumeshachimba kinachofuata sasa ni hatua za usambazaji. Mradi huo ulioutaja ujenzi wake mara tukipata fedha tunakuja kuanza mara moja.

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga mradi mpya wa maji safi na salama kuliko kuendelea na ukarabati wa Mradi wa Kata ya Kihurio ambao ulijengwa mwaka 1967?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, ningependa kujua mpango wa Serikali kutumia chanzo cha maji ya Ziwa Nyasa kuhudumia wananchi wa Kata ya Ruhuhu na Manda kwa sababu wananchi hawa wanaliwa sana na mamba hasa Kitongoji cha Panton?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Kamonga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, matumizi ya Ziwa Nyasa kama chanzo endelevu tayari tuna miradi ambayo tumeanza kuitekeleza ukanda wa Nyasa pamoja na Ruhuhu. Tunafahamu eneo ambalo wananchi walikuwa wakiliwa na mamba na tayari tulishaagiza RM Njombe ameanza usanifu na anakuja kutekeleza.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga mradi mpya wa maji safi na salama kuliko kuendelea na ukarabati wa Mradi wa Kata ya Kihurio ambao ulijengwa mwaka 1967?

Supplementary Question 4

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kuiuliza Serikali; je, ni lini italeta mradi wa maji kwenye Tarafa ya Ngerengere?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Taletale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Ngerengere ipo kwenye mpango wa Wizara, Mheshimiwa Waziri alishapita maeneo hayo. Mheshimiwa Mbunge tuko mbioni kuleta mradi huu wa maji tutatumia Mradi wa Chalinze ama Morong’anya kuhakikisha maji yanafika Ngerengere.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga mradi mpya wa maji safi na salama kuliko kuendelea na ukarabati wa Mradi wa Kata ya Kihurio ambao ulijengwa mwaka 1967?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, zaidi ya 85% ya wakazi wa Wilaya ya Muleba hawana maji safi na salama; je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwa ajili ya Wilaya ya Muleba?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oscar, Mbunge wa Muleba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi ule wa mradi kutoka Ziwa Victoria upo kwenye mpango wa Wizara. Mara tutakapopata fedha tutaendelea kuzileta kwa mafungu ili mradi huu tuanze kuutekeleza.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga mradi mpya wa maji safi na salama kuliko kuendelea na ukarabati wa Mradi wa Kata ya Kihurio ambao ulijengwa mwaka 1967?

Supplementary Question 6

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi.

Ni lini Serikali itatekeleza maelekezo ya Waziri Mkuu ya kupeleka maji Kijiji cha Mtunduwalo iliyothibitishwa kwamba maji yale sasa hayawezi kutumika kwa matumizi ya binadamu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kapinga, Mbunge wa Mbinga Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maelekezo ya viongozi wakuu yote tunayatekeleza na suala hili la kupeleka maji Ruanda nalo pia lipo kwenye utaratibu wa kuona kwamba hivi punde tunakuja kuhakikisha maji Ruanda yanaletwa.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga mradi mpya wa maji safi na salama kuliko kuendelea na ukarabati wa Mradi wa Kata ya Kihurio ambao ulijengwa mwaka 1967?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante; swali langu ni je, ni lini Serikali itafanya tathmini ya utekelezaji wa miradi ya maji kwenye Kata za Mwika Kaskazini, Mamba Kaskazini, Marangu Mashariki, Mwika Kusini na Kilemu kwa sababu miradi hiyo ina matatizo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Charles Kimei, Mbunge wa Vunjo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge, maeneo hayo yote uliyoyataja tuna miradi ambayo inaendelea na usanifu na miradi ambayo tunaitafutia fedha na katika mgao ujao na hata Jimbo la Vunjo nalo litakuja kupatiwa fedha ili miradi hii ianze kutekelezwa kwa wakati.

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga mradi mpya wa maji safi na salama kuliko kuendelea na ukarabati wa Mradi wa Kata ya Kihurio ambao ulijengwa mwaka 1967?

Supplementary Question 8

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa nataka kujua ni lini mradi mkubwa wa maji kutoka Wilaya ya Ileje, Mto Songwe kwenda Jimbo la Tunduma utaanza kutekelezwa? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mradi huu ni mradi mkubwa na tayari umeshaanza utekelezaji kwa hatua za awali na tunatarajia maji Tunduma yatafika kwa sababu ni mradi ambao unajengwa kwa awamu.