Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 125 2023-02-09

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga mradi mpya wa maji safi na salama kuliko kuendelea na ukarabati wa Mradi wa Kata ya Kihurio ambao ulijengwa mwaka 1967?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anne Kilango, Mbunge wa Same Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kujenga mradi mkubwa utakaoondoa kabisa tatizo la maji katika Kata ya Kihurio ambapo kwa sasa usanifu unaendelea na ujenzi utafanyika katika mwaka wa fedha 2023/2024.

Aidha, katika kupunguza kero ya uhaba wa maji, Serikali kushirikiana na Jumuiya ya Watumiaji Maji inaendelea kufanya ukarabati mdogo wa miundombinu ya maji kwenye Kata ya Kihurio. (Makofi)