Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na napongeza sana Serikali ya Awamu ya Sita kwa maboresho makubwa, hata hivyo nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, moja; ni lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha hasa madaktari na wauguzi?

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili; ni lini Serikali itapeleka vifaa vya kutosha katika Kituo cha Afya Chimara lakini pia Kituo cha Afya Igurusi ili waweze kutoa huduma za upasuaji? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Jimbo la Mbarali, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshapeleka vifaa tiba vya shilingi milioni 418 katika Halmshauri ya Mbarali, lakini katika mwaka huu wa fedha Serikali imetenga shilingi bilioni 69.65 kwa ajili ya kupeleka vifaa tiba kwenye vituo vya afya na hospitali za halmashauri pamoja na zahanati zilizokamilika. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba zoezi la kupeleka vifaa tiba kwenye vituo vyetu ni endelevu, lakini pia vituo hivi vya Mbarali vitapata vifaa tiba hivyo.

Mheshimiwa spika, lakini pili katika mwaka wa fedha uliopita Serikali iliajiri watumishi 10,462 na Halmashauri ya Mbarali ilipata watumishi 51 wakiwemo madaktari na wauguzi na Seriakli itaendelea kupeleka watumishi hao katika halmashauri zote nchini ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, ahsante.

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Supplementary Question 2

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Mapera kilichopo Mbinga Vijijini hakina vifaa tiba vya msingi ikiwemo ultrasound, x-ray na hamna generator hali inayozorotesha upasuaji hasa nyakati za usiku. Fedha ambazo Serikali imetenga, je, na Kituo cha Afya cha Mapera kimetengewa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Judith Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kituo hiki cha afya cha Mapera kilichopo katika Halmashauri ya Mbinga ni moja ya vituo ambavyo vimeingia kwenye orodha ya kupelekewa vifaa tiba katika bajeti ya mwaka wa fedha huu 2022/2023, lakini pia tutaendelea kutenga katika bajeti ijayo ya 2023/2024, ahsante.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Supplementary Question 3

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi.

Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba mfano x-ray machine na ultrasound kwenye Vituo vya Afya vya Kamsamba, Mkulwe, Msangano, Ndalambo pamoja na Kapere?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester Sichalwe, Mbunge wa Jimbo la Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa taratibu na sera za afya, vituo vya afya vinapelekewa mashine za ultrasound lakini vituo vya afya ambavyo vinapata mashine za x-ray ni baada ya tathmini ya kuona idadi ya wananchi wanaotibiwa katika maeneo hyo.

Kwa hiyo, naomba nichukue hoja ya Mheshimiwa Mbunge, tufanye tathmni ya kuona idadi ya wananchi wanaotibiwa kaita Kituo cha Kamsamba na vingine ambavyo amevitaja kama vinakidhi sifa za kuwa na mashine za x-ray, lakini nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Momba kwamba mashine za ultrasound ziko ndani ya uwezo wa halmashauri kununua wakati Serikali inaendelea kutafuta fedha kuongeza nguvu katika maeneo hayo, ahsante.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Supplementary Question 4

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kumekuwa na mkanganyiko kwa hizo pesa zilizopelekwa katika halmashauri kwa sababu wengine hawajui kama ziende kwenye vituo vya afya au kwenye zahanati.

Sasa Serikali haioni sababu ya kuweka maelekezo maalum kabisa kwamba hizi pesa either ziende kwenye kituo cha afya na hizi ziende kwenye zahanati?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mchungahela, Mbunge wa Jimbo la Lulindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inapopeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa zahanati au vituo vya afya au hospitali za halmashauri inapeleka na barua ya maelekezo kwa Mkurugenzi kwamba fedha zilizoletwa ni kwa ajili ya kujenga kituo cha afya eneo gani au zahanati eneo gani au hospitali ya halmashauri eneo gani?

Kwa hiyo, naomba nirudie kusisitiza kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kwamba wazingatie maelekezo yanayotolea na Ofisi ya Rais, TAMISEMI mara fedha zinapopelekwa katika ujenzi wa vituo hivi, ili kuepuka mkanganyiko ambao Mhehimiwa Mbunge ameusema, ahsante.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Supplementary Question 5

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika,
ahsante sana kwa kunipa fursa.

Kituo cha afya cha Umbwe ambacho ni ndio kituo pekee cha afya katika Tarafa ya Kibosho hakina gari la kubeba wagonjwa; je, Serikali ina mpango gani wa kutupatia gari la kubeba wagonjwa katika kituo hiki?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Profesa Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimia Spika, ni kweli kwamba Kituo cha Afya cha Umbwe ni kituo pekee katika tarafa hiyo na kinahudumia wananchi wengi na hakina gari la wagonjwa. Mheshimiwa Ndakidemi amekuwa akifuatilia mara kwa mara, lakini naomba nikujulishe Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mwaka huu wa fedha tutapeleka magari ya wagonjwa katika halmashauri zote 184, lakini pia tutapeleka magari ya huduma za afya kwa maana usimamizi katika halmashauri zote 184, ikiwemo Halmashauri hii ya Moshi Vijijini, na hivyo ni maamuzi ya halmashauri kuona inakipa kipaumbele kituo hiki cha afya cha Umbwe ili kiweze kupata gari hilo, ahsante.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Supplementary Question 6

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante; je, ni lini Serikali hii itapeleka vifaa tiba katika Kituo cha Afya cha Bashnet na Madunga katika Jimbo la Babati Vijijini ambavyo viko tayari?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, pamoja na Kituo hiki cha Afya cha Bashnet, lakini na vituo vingine vya afya ambavyo vimekamilika katika Jimbo la Babati Vijijini Serikali imetenga fedha shilingi bilioni 69.95 katika mwaka huu wa fedha na tayari vifaa tiba vimeanza kupelekwa. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutatoa kipaumbele pia katika kituo hiki cha afya ili kiweze kupata vifaa tiba hivyo, ahsante.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Supplementary Question 7

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na naishukuru Serikali kwa kutujengea vituo vya afya ndani ya Jimbo la Hai.

Swali langu, ni lini sasa Serikali itatuletea vifaa tiba kwenye Vituo vya Afya vya Kwansira, Chemka na pale Kisiki?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nafahamu kwamba Kituo cha Afya cha Kwansira ambako mimi na yeye tulifanya ziara na kazi ya ujenzi iko hatua za mwisho, ni sehemu ya vituo ambavyo vinahitaji vifaa tiba mara baada ya kukamilika, lakini pamoja na hivi vituo vya afya vingine ambavyo amevitaja. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendelea kutenga fedha na kupeleka vifaa tiba kwenye vituo hivyo alivyovitaja ili kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi wa Hai, ahsante.

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Supplementary Question 8

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante, Kituo cha Afya cha Igalula katika bajeti tulikitengea milioni 450 na tumekwisha pokea milioni 450 lakini cha ajabu TAMISEMI mmeleta barua ya kugawa zile fedha kwenye vituo vitatu.

Je, kwa nini Serikali isione haja ya kukimaliza kabisa Kituo cha Afya cha Igalula katika vifaa tiba na kiendelee kutoa huduma stahiki? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant David Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inapopeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya kwanza dhamira ya kwanza ni kuhakikisha kwamba vituo vile vinakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi mara moja.

Naomba sasa niichukue hoja ya Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imepeleka shilingi milioni 450 lakini kuna maelekezo ya kuzigawa fedha hizo katika vituo vitatu, nikitoka hapa nikaa na Mheshimiwa Mbunge lakini nifuatilie kuona sababu za msingi za kufanya hivyo na kama hakuna sababu tutakubaliana tukamilishe Kituo cha Afya cha Igalula na hatimaye tuendelee na vituo vingine kwa mujibu wa utaratibu, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Supplementary Question 9

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwanza, nimpongeze sana Mheshimiwa Jenista kwa kazi nzuri anayoifanya katika kile kijiji kwenye zahanati.

Je, ni lini sasa Serikali mtapeleka vifaa tiba kwenye Zahanati ya Mdunduwaro ili ianze kufanya kazi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika,
ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Ntara lakini nimpongeze sana Mheshimiwa Jenista Mhagama kwa namna ambavyo wameendelea kusimamia ujenzi wa Zahanati ya Mdunduwaro na ni kweli kwamba Mheshimiwa Jenista Mhagama amekuwa akilifuatilia na Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara amekuwa akilifuatilia.

Nimhakikishie kwamba tulishakubaliana kwamba kwanza Zahanati ile ikamilike kabla ya tarehe 30 Machi, isajiliwe, lakini tumeshakubaliana vifaa tiba vitapatikana ndani ya halmashauri kwa sababu tayari wana vifaa ambavyo havitumiki katika vituo vingine, lakini na Serikali itaongezea kuhakikisha kwamba kinaanza kutoa huduma, ahsante.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Supplementary Question 10

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali.

Kituo cha Afya cha Upugi kilikarabatiwa kwa hali ya juu sana na kuletewa mitambo ya kisasa, lakini hela zilipungua kwa kujengea jengo la mashine ya x-ray na ultrasound. Huu mwaka wa nne zile mashine hazijafunga.

Je, lini Serikali itajenga jengo la kuweka mashine ya x-ray na ultrasound katika Kituo cha Upugi? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Almas Maige, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ikipeleka fedha katika ujenzi wa miundombinu ya huduma za afya, kwanza tunapeleka kwa awamu. Awamu ya kwanza, majengo ya OPD, majengo ya maabara ya mama na mtoto; lakini awamu ya pili tunatenga majengo mengine ya Vipimo ya x-ray, ultrasound na wodi, lakini kwa taarifa ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitoa kwamba fedha hazikutosha kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya x-ray na ultrasound, nimhakikishie kwamba Serikali kwa maana ya fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri na Serikali Kuu tutakaa tuone wapi tunapata fedha ili tuweze kukamilisha majengo hayo, ahsante. (Makofi)

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Supplementary Question 11

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Nakapanya, jengo la upasuaji limekamilika na baadhi ya vifaa vya upasuaji vipo na ambulance ipo.

Je, ni lini Serikali itakamilisha baadhi ya vifaa vya upasuaji ili kituo kile kianze kutoa huduma ya upasuaji na kumsaidia mama na mtoto katika kituo kile? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kungu, Mbunge wa Tunduru Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya hiki cha Nakapanya ni kweli kwamba kuna baadhi ya vifaa tiba vimeshafika, lakini tayari tumepanga watumishi kwa ajili ya kuanza kutoa huduma na tunafahamu kwamba kuna baadhi ya vifaa tiba hasa kwenye jengo la upasuaji bado havijafika.

Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye bajeti ya mwaka huu, vituo vyote hivi vya afya vilivyokamilika ikiwemo hiki cha Nakapanya kimetengewa fedha kati ya ile shilingi bilioni 69.95 kwa ajili ya kupeleka vifaa tiba ili vianze kutoa huduma za upasuaji kwa wananchi, ahsante.