Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 122 2023-02-09

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Jimbo la Mbarali, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita imefanya maboresho makubwa ya miundombinu katika sekta ya afya ikiwemo ujenzi wa hospitali za halmashauri, vituo vya afya na zahanati.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imepeleka vifaa na vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 418 kwa ajili ya jengo la huduma za dharura (EMD), pamoja na mashine ya kisasa ya X-ray ya shilingi milioni 155 hospitali ya Wilaya ya Mbarali.

Mheshimiwa Spika, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 69.95 katika bajeti ya mwaka 2022/2023 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa na vifaa tiba kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini ikiwemo Hospitali ya Halmashauri ya Mbarali ambayo imetengewa shilingi milioni 100, ahsante.