Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya upanuzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Licha ya majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili madogo. Swali la kwanza; licha ya mpango mzuri na unaoendelea wa upanuzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro lakini kuna mpango wa kujenga Hospitali ya kisasa ya Rufaa ya Mkoa wa Hospitali ya Morogoro.

Je, ni lini ujenzi huu utaanza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika Kituo cha Mafiga Manispaa ya Morogoro wanawake wengi wajawazito wanapenda sana kujifungulia kwenye kituo hicho lakini tatizo mojawapo linalojitokeza kituo hiko hakina jengo la upasuaji.

Je, kuna mpango gani wa kuweka jengo la upasuaji katika Kituo hicho cha Mafiga? Ahsante sana.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Mbunge nikupongeze. Unakumbuka ulikuja na ukaniambia na tulikwenda hospitali ya mkoa na uliona miundombinu na uwekezaji mkubwa ambao umefanyika kwenye hospitali yenu ya mkoa. Najua lengo lenu, pamoja na upanuzi unaozungumziwa kwenye eneo hili la hospitali mnahitaji kujenga hospitali nyingine eneo lingine. Mimi nikuombe, kama nilivyosema hapa, majadiliano yanayoendelea kati ya Wizara na Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro tukiyamaliza basi tutakaa pamoja ili tuweze kwenda forward tukiwa pamoja. Kwa sababu sasa hivi nikikupa majibu inawezekana huo mchakato wa kimkoa wakawa na mawazo mengine tofauti na hayo ambayo wewe unayo. Kwa hiyo tutashirikiana kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili unazungumzia kwamba pale kwa akina mama hakuna jengo la upasuaji. Mheshimiwa Mbunge naomba nikimaliza hili swali tukae mimi na wewe tukae na TAMISEMI tuweke mkakati wa pamoja tuhakikishe hicho unachokisema kinaenda kutokea.

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya upanuzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 2

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Naomba nitumie nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Serikali anayoiongoza kwa kutupatia fedha za kumalizia jengo la mtoto katika Hospitali ya Mkoa wa Kilimanjaro, Hospitali ya Mawenzi. Tangu alipoitembelea Octoba 2021 fedha zimekuwa zikija na fedha za UVIKO zimekuja, na sasa jengo lile linamalizika. Sasa swali langu ni;

Je, ni lini Serikali itaanza mpango wa kuitengeneza master plan ya hospitali ile upya ili kuondoa yale majengo ya zamani na kuweka majengo mapya ya ghorofa yanayoendana na hospitali za kisasa?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimwambie Mbunge Rais wetu Daktari Samia Suluhu Hassan alipotembelea pale Hospitali ya Mawenzi yeye aliomba mambo kadhaa na mambo hayo Rais wetu ameshatoa hela. Aliomba bilioni sita ya kumalizia jengo la mama na mtoto na tayari bilioni sita zimekwenda. Pia aliomba CT-Scan, tayari imekwenda, aliomba bilioni 1.3 kwa ajili ya emergency department imeshajengwa na bilioni 1.3 imekwenda, na jana zimekwenda bilioni moja kwa ajili ya kuendeleza kazi ambayo unasema kwamba kubomoa yale majengo ya zamani na kunyanyua mengine ambayo yatafanya ile hospitali iwe vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna moja tu ambalo tunaenda kutekeleza kabla ya Juni mwaka huu ambalo ulimwomba Mheshimiwa Rais; la ujenzi wa Kiwanda cha kuzalisha gesi tiba, hilo litaenda kutekelezwa kabla ya Juni na kazi itaenda pale vizuri sana. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie kazi uliyomwomba Rais inaendelea kufanyika na ahadi amezitekeleza takriban zote. (Makofi)

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya upanuzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Hospitali ya Rufaa Mkoani Rukwa kwa sababu tayari uwanja ulishapatikana na ufundi sanifu ulishafanyiwa. Je, ni lini Serikali sasa itaanza ujenzi wa hospitali hiyo? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namwelewa anachosema na usanifu ni kweli umefanyika kama Mheshimiwa Mbunge anavyosema. Kwanza nimpongeze kwamba anafatilia masuala mazima ya afya ya hopsitali yao ya mkoa. Kwa mwaka huu zimetengwa bilioni 5.5 kwa ajili ya hospitali anayosema na usanifu anaouzungumzia unaenda kufanyika.