Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 115 2023-02-08

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafanya upanuzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2021/2022 na 2022/2023, Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya upanuzi wa miundombinu ya majengo ya huduma za dharura, huduma za wagonjwa mahututi, huduma za mionzi ambapo majengo haya yamekamilika na yanatumika. Pia ununuzi wa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.8, umefanyika. Pamoja na maboresho hayo, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 350 kwa ajili ya umaliziaji wa jengo la upasuaji wa mifupa ambapo jengo hili litakamilika mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara inaendelea kushirikiana kwa karibu na Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya usanifu wa majengo yanayokusudiwa kujengwa ikiwa ni sehemu ya mpango wa upanuzi wa hospitali hii.