Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kudhibiti kuhama kwa Mto Ruvu-Kibaha ili kuzuia uharibifu wa mashamba na miundombinu ya Reli ya SGR?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niipongeze Serikali kwa majibu mazuri, lakini niongezee nyongeza moja kwamba hadi leo hii lile eneo ambalo tulilizungumza na liliuliziwa swali, Serikali imetekeleza vizuri na limeziba lile eneo, kwa hiyo tunawapongeza sana. Swali moja dogo la nyongeza; kwa kuwa wakulima wa bonde hilo walikuwa wanazuiwa kuendeleza shughuli zao za kilimo katika maeneo hayo kutokana na Mto Ruvu kupungua kasi yake ya maji na sasa eneo lile limeshazibwa.

Je, Serikali inampango gani sasa wa kuwasaidia wakulima wale waendelee na shughuli zao za umwagiliaji mdogo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nipende kushukuru kwa kupongeza jitihada kubwa ambayo taasisi ya DAWASA imeweza kufanya na sasa maji hayatapakai tena. Vile vile Serikali ina mipango mbalimbali kuhakikisha suala la maji kuchepuka kutoka kwenye mto tunakwenda kulidhibiti. Hili tutalifanya kwa kutumia Bonde la Maji ya Wami-Ruvu na tayari wameshapata mhandisi mshauri ambaye anafanya usanifu kwa ajili ya kujenga bomba kuu moja ambalo wananchi watapaswa kujiunga katika kikundi kimoja ili waweze kuhudumiwa kwa sehemu moja halafu wao sasa ndio watachepusha kwenye maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuipatia Wizara fedha. Tayari tumeshaingiza mitambo ya kuchimba mabwawa na tunatarajia kama Wizara tuweze kuchimba mabwawa madogo madogo ambayo nyakati za mvua tutaweza kuvuna maji, tutayahifadhi pembezoni mwa mto huko ili wananchi waweze kuja kuyatumia kwa ajili ya umwagiliaji na wasiweze kudhuru mto katika shughuli za kuleta chanzo cha maji kwa shughuli za kibinadamu.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kudhibiti kuhama kwa Mto Ruvu-Kibaha ili kuzuia uharibifu wa mashamba na miundombinu ya Reli ya SGR?

Supplementary Question 2

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Vijiji vya Changarawe katika Kata ya Masanze na Vijiji vya Malangali, Muungano, Mamoyo, Kibaoni na Maluwi katika Kata za Tindiga na Mabwerebwere mito yake imepoteza mwelekeo, inahatarisha maisha ya watu. Sasa nilikuwa naomba kuuliza Serikali;

Je, ni madhara kiasi gani kwa wananchi wetu yatokee ili Serikali ichukue hatua?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, aaomba kujibu swali la Mheshimiwa Dennis Londo (Mb) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba, ni kiasi gani cha madhara ili Wizara iweze kuchukua hatua. Wizara hatusubiri madhara lakini tayari tunachukua hatua kwa kutimiza majukumu yetu kuhakikisha maji hayawi laana, maji ni neema. Maeneo ambayo maji yanachepuka na kusababisha maeneo ya wananchi kuvamiwa tayari tumeyapa kipaumbele. Kwa maeneo aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge, hasa Mto Miombo ambao unasababisha madhara kwenye kata alizozitaja ya Masaza, Masava na nyingine tayari mkandarasi yupo site anafanya utafiti. Lengo ni kuona maeneo yote ambayo yanaathirika na maji yanapochepuka kwenye mto hasa nyakati za masika tunakwenda kuyadhibiti, yanaenda kutumika vizuri kwa shughuli za kibinadamu. Shughuli ambazo zinafanyika na wananchi hawa za mboga mboga, kilimo kidogo kidogo basi yote yatajengewa miundombinu rafiki ili kulinda mto kwa sababu kulinda vyanzo vya maji ni jukumu letu sote.