Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 113 2023-02-08

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kudhibiti kuhama kwa Mto Ruvu-Kibaha ili kuzuia uharibifu wa mashamba na miundombinu ya Reli ya SGR?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Michael Costantino Mwakamo Mbunge wa Kibaha Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mto Ruvu eneo la Kibaha hadi Bagamoyo umekuwa na kawaida ya kuhamahama kwa vipindi tofauti tofauti kutokana na kuwa katika uwanda wa chini karibu na Bahari ya Hindi. Hali hii hupunguza kasi na kufanya udongo kutuwama ndani ya mto na kusababisha mto kuhama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea na kazi ya kunyoosha mto pamoja na kuimarisha kingo zilizoathiriwa kwa kuweka gabions na njia mbalimbali, ikiwemo upandaji wa miti pembezoni mwa mto na kwenye vyanzo vya maji, kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa kuhifadhi vyanzo vya maji, kuiwezesha jamii kutekeleza shughuli mbalimbali za kujipatia kipato ili kuondoka ndani ya vyanzo vya maji. Kuweka alama na mipaka na mabango ya makatazo ya kuzuia kufanya shughuli za kibinadamu ndani ya hifadhi ya vyanzo vya maji ili kurudisha uoto wa asili na kupunguza athari za mmomonyoko. Jitihada hizi zitaepusha mashamba katika eneo hilo kuathiriwa na maji ya mto Ruvu.