Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE K.n.y. MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuweka taa za barabarani katika Miji ya Magu, Kisesa, Nyanguge, Lugeye na Ilungu?

Supplementary Question 1

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Niishukuru sana Serikali kwa mpango iliyoweka, tuiombe sasa tu zabuni iwahi na mkandarasi apatikane ili wanachi wanufaike na taa hizi za barabarani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina swali moja tu la nyongeza mahali hapa. Ni nini sasa Mkakati wa Serikali ya uwekaji wa taa za barabarani kwenye miji iliyoendelea ikiwemo Magu, Busega pale Masanza pamoja na Nasa Ginnery lakini pamoja na Itilima Mkoani Simiyu? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Simon Songe, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nitoe tu maelezo kwa ajili ya swali hili. Kwamba kwa sasa Serikali imetoa mamlaka kwa Mameneja wa Mikoa wote wa TANROADS kupitia mikutano ya mifuko ya barabara pamoja na RCC kuanisha miji yote mikubwa ambayo imekua na inahitaji taa ili waweze kuziombea hela kwa ajili ya kuweka barabara kwenye miji yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa sasa kwa barabara zote ambazo zinajengwa kwa sasa imekuwa ni sehemu ambapo tunapoanza kujenga barabara miji yote inawekewa taa. Kwa hiyo inakuwa ni sehemu ya gharama ya zile barabara. Kwa hiyo ni pamoja na hiyo miji aliyoisema Mheshimiwa Simon Songe, ahsante.

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE K.n.y. MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuweka taa za barabarani katika Miji ya Magu, Kisesa, Nyanguge, Lugeye na Ilungu?

Supplementary Question 2

MHE. ANTON A. MWANTONA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi lakini pia namshukuru Rais wa Jamhuri wa Tanzania alipofanya ziara katika Jimbo langu la Rungwe aliahidi kuweka taa katika Mji Kiwila, Mji mdogo wa Tukuyu pamoja na Ushirika.

Je, ni lini sasa taa hizo zitawekwa katika miji hiyo ambayo nimeitaja?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantona, Mbunge wa Rungwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hivi tunavyoongea miji ya Kiwila, Tukuyu na Ushirika itawekewa taa; na sasa hivi Mkandarasi ameshapatikana, wako kwenye hatua za mobilization, ahsante.

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE K.n.y. MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuweka taa za barabarani katika Miji ya Magu, Kisesa, Nyanguge, Lugeye na Ilungu?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kunapokuwa na taa za barabarani kwanza kuna kuwa na usalama wa wasafiri lakini vile vile wananchi wanafanya shughuli zao za uchumi mpaka usiku kwa sababu kuna usalama.

Je, ni lini Miji ya Hedaru, Makanya, Mji mdogo wa Same, Njoro Kisiwani pamoja na Mwembe watawekewa taa za barabarani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa David Mathayo David, Mbunge wa Same, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, miji aliyoitaja, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kilimanjaro ameshawasilisha maombi na tunategemea fedha itaenda mwaka huu ili miji hiyo iweze kuwekewa taa kwa ajili ya usalama lakini pia na kupendeza miji aliyoitaja, ahsante.

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE K.n.y. MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuweka taa za barabarani katika Miji ya Magu, Kisesa, Nyanguge, Lugeye na Ilungu?

Supplementary Question 4

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa tarehe 22 Mwezi wa Nane 2022 Serikali ya kuanza kujenga Barabara ya Morogoro – Njombe boarder kwa kiwango cha kilometa 100 kutoka Ifakara kwenda Chita.

Je, Wananchi wa Mlimba wangependa kujua taa inaweza kuwa component kwenye tenda hasa kwenye maeneo ya miji kama Mchombe na Mgeta na Mlimba Mjini? Ahsa nte.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kunambi, Mbunge wa Mlimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwa sasa barabara zote ambazo tunazi – design na kuzijenga, miji yote ambayo inapitiwa na hiyo barabara inawekewa taa. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Mlimba, kwamba miji yote ambayo itapitiwa na hiyo barabara kilometa 100 taa itakuwa ni sehemu ya hiyo kandarasi, ahsante.