Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 110 2023-02-08

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE K.n.y. MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuweka taa za barabarani katika Miji ya Magu, Kisesa, Nyanguge, Lugeye na Ilungu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniventura Destery Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Wakala wa Barabara Tanzania Mkoa wa Mwanza umepanga kuweka taa katika Miji ya Magu, Kisesa, Nyanguge, Lugeye na Illungu. Uchambuzi wa zabuni kwa ajili ya kumpata mkandarasi unaendelea na unatarajiwa kukamilika tarehe 15 mwezi Februari mwaka huu wa 2023 na kazi inatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu wa 2023, ahsante.