Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Kata za Mtungulu, Mwamashiga, Isakamaliwa, Kining’inila na Kinungu zitapatiwa umeme?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Awali matarajio ya Serikali ilikuwa ni kuhakikisha maeneo haya ya vijiji vinawaka umeme ilipofika mwezi wa 12 mwaka jana, mwaka 2022, na ambapo ndio muda wa mkandarasi kukaa site ulikuwa unakamilika. Hata hivyo, mpaka ninapoongea hivi sasa, hivi vijiji maeneo mengi mashimo yamechimbwa na nguzo zimelazwa chini bado hazijasimamishwa.

Je, naomba kujua kauli ya Serikali; ni lini, hivi vijiji vitawashwa umeme kwa kuwa na muda wa mkataba wa mkandarasi umeshakwisha?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nicholaus Ngassa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna mikataba iliyotakiwa kuisha Disemba mwaka jana. Hata hivyo, kama tunavyofahamu, tulipata changamoto ya kuongezeka kwa gharama za vifaa kipindi ambacho kulikuwa na magonjwa ya UVIKO. Pamoja na hayo tumepata faida nyingine ya kupata ongezeko la kilometa mbili kwa kila kijiji ambacho kilitakiwa kupelekewa umeme. Kwa hiyo vijiji vilivyo vingi upelekaji wa umeme utakamilika kufikia mwezi Disemba mwaka huu 2023. Kama nilivyosema kwenye majibu ya msingi kwenye baadhi ya maeneo kwa Mheshimiwa Ngassa, mwezi Aprili mwaka huu kuna maeneo ambayo tayari yatakuwa yamefikiwa na umeme kwa kadri alivyoiliza.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Kata za Mtungulu, Mwamashiga, Isakamaliwa, Kining’inila na Kinungu zitapatiwa umeme?

Supplementary Question 2

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipatia nafasi. Naomba kuiuliza Serikali;

Je, ni lini vijiji 63 vilivyopo katika Jimbo la Newala Vijijini ambavyo havijawahi kuona umeme kabisa vitapatiwa umeme ili nao wawe wanufaika wa nishati hii muhimu? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maimuna Mtanda, Mbunge wa Newala Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mhehsimiwa Mwenyekiti, wakandarasi katika Mkoa wa Mtwara na Lindi wako kazini wananendelea. Tumehimizana na wakandarasi walio katika maeneo hayo na kufatiliana nao kwa wakati ili kuhakikisha kazi yao inakamilika. Kama nilivyosema, ile kazi ya nyongeza na ya awali itakamilika mwezi Disemba mwaka huu 2023.

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Kata za Mtungulu, Mwamashiga, Isakamaliwa, Kining’inila na Kinungu zitapatiwa umeme?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Ukosefu wa copper wire na mita ni moja ya sababu inayochelewesha uunganishwaji wa umeme katika Jimbo la Muhambwe, ikiwemo kata ya Busagara, Kitahara, Kumsenga na Mlungu;

Je, ni lini Serikali italeta vifaa hivi, ili kata hizi ziweze kunufaika na kuunganishiwa umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Florence Samizi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa uzalishaji wa vifaa ulitokea katika maeneo mengi baadaya kupata matatizo ya UVIKO, na hivyo milango ilivyofunguliwa order zilikuwa nyingi na wahitaji walikuwa wengi, Kwa hiyo na sisi tunahakikisha tunatoa order za kutosha na kwa kadri zinavyozaliswha tunazipata. Nimuhakikishie tu Mheshimiwa Samizi kwamba, katika eneo lake na maeneo mengine vifaa vitapatikana na huduma kwa wananchi itaendelea kuunganishwa kwa sababu pesa tunayo na tunaendelea kufatilia kwa ajili ya upatikanaji wake.