Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 117 2023-02-08

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: -

Je, ni lini Kata za Mtungulu, Mwamashiga, Isakamaliwa, Kining’inila na Kinungu zitapatiwa umeme?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nicholaus George Ngassa, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata za Mtungulu, Mwamashiga, Isakamaliwa, Kining’inila na Kinungu zote zipo kwenye Mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili unaoendelea. Mkandarasi anayetekeleza mradi huo anaitwa M/S CEYLEX ameshafika kwenye maeneo hayo. Kwa Kata ya Mtunguli, katika vijiji viwili kati ya vijiji vitatu ambavyo ni Maguguni na Mtungulu, kazi ya kusambaza umeme imekamilika na umeme umeshawashwa, isipokua Kijiji cha Mwajijambo ambacho kazi ya kuvuta nyaya inaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa Kata za Mwamashiga, Isakamaliwa, Kining’inila na Kinungu kazi ya uchimbaji mashimo na usimikaji nguzo inaendelea. Utekelezaji wa miradi hii yote unategemewa kukamilika ndani ya kipindi cha mkataba ambacho kinaishia mwezi Aprili, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.