Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mbinga Luwaita kupitia Mradi wa Agri-connect kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza nishukuru sana kwa majibu ya Serikali lakini nilikuwa na ombi. Naiomba Serikali kuhakikisha kwamba mradi huu unatekelezwa mapema kwa sababu ni barabara muhimu sana kwa wananchi wa kata ya Luwaita kwa ajili ya kusafirisha mazo yao kwenda kwenye maeneo ya soko, ahsante sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Jonas William Mbunda, Mbunge wa Mbinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepokea tutafanya hivyo, kwa sababu awamu ya kwanza na ya pili ziko katika utekelezaji kwa hito na hii ya tatu tutaitekeleza, ahsante.

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mbinga Luwaita kupitia Mradi wa Agri-connect kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa menyekiti, ahsante kwa swali lanyongeza. Barabara ya kutoka Mapera kuelekea Ilela iliyopo Mbinga Vijijini imeharibika sana na kukwamisha shughuli za maendeleo za wakazi wa Kata za Mapera, Kambarage pamoja na Mikaranga.

Je, Serikali ina mkakati gani wa dharura kwa ajili ya kurekebisha barabara hii ili wakazi wa maeneo haya shughuli zao za maendeleo ziweze kuendelea?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Judith Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, niagize tu TARURA mkoa wake waende waipitie hii barabra ya Mapera mpaka Ilela waangalie uharibifu ambao upo na watoe tathmini ili tutafute fedha iweze kurekebishwa, ahsante sana.