Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 106 2023-02-08

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mbinga Luwaita kupitia Mradi wa Agri-connect kwa kiwango cha lami?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jonas William Mbunda Mbunge wa Mbinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Agri-connect ni programu inayofadhiliwa na Jumuiya ya Umoja wa Ulaya ambapo inahusisha ujenzi wa barabara kwa lengo la kusafirisha mazao kutoka shambani au sehemu za uzalishaji kwenda kwenye masoko, viwanda na maghala. Aidha, utekelezaji wa mradi huu utafanyika kwa awamu Tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti barabara ya Luwaita ipo katika Awamu ya Tatu ya programu ya Agri-connect itakayoanza mwaka wa fedha 2023/2024. Kwa sasa, awamu ya tatu ipo kwenye hatua ya uainishaji, uhakiki na upangaji wa vipaumbele vya barabara katika mikoa sita, ambayo ni Iringa, Njombe, Ruvuma, Mbeya, Katavi na Songwe kwa kusimamiwa na Wizara ya kilimo.