Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi ili kuondoa migogoro ya Wakulima na Wafugaji katika Wilaya ya Kilwa?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nakushukuru Mheshimiwa Waziri kwa kunijibu swali langu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ningependa kumuuliza Mheshimiwa Waziri; kwamba kutokanana changamoto kuwa kubwa ya migogoro ya wakulima na wafugaji kila kukicha ambayo imesababisha watu mbalimbali kupambana na kufa wengine, wengine wamepata ulemavu.

Je, haioni kwamba kuna uhitaji sasa wa kuharakisha huu mpango wa matumizi bora ya ardhi, ili vijiji bora 34 vilivyobaki viweze kumalizwa kupangwa katika huu mpango wa matumizi bora ya ardhi mwaka 2023/2024?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swalli la pili. Katika kipindi cha miaka 10 Takwimu za Sensa zimeonesha katika Wilaya ya Kilwa kumekuwa na ongezeko kubwa la wananchi. Mwaka 2012 tulikuwa na wananchi 190,744, mwaka 2022 takwimu za sensa zinaonesha kwamba wananchi wa Wilaya ya Kilwa wameongezeka hadi kufikia 297,676 sawa na ongeezeko la watu 106,932 sawa na asilimia 52 ya ongezeko. Kutokana na ongezeko hili ni wazi kwamba sehemu kubwa ya watu walioongezeka ni jamii ya wafugaji...

MWENYEKITI: Uliza swali.

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Je, Serikali haioni sasa wakati umefika wa kuweza kuwahamisha baadhi ya wafugaji kutoka Wilayani Kilwa kwenda maeneo mengine ya nchi kama ilivyofanya katika Bonde la Ihefu na katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kuna changamoto ya mogogoro kati ya wafugaji na wakulima katika Halmashauri ya Kilwa, lakini pia katika baadhi ya halmashauri hapa nchini. Serikali imeendelea kuchukua hatua, na hatua moja muhimu ni kupanga matumizi bora ya ardhi katika vijiji ili kuwa na maeneo mahsusi kwa ajili ya kilimo, pamoja nakuwa na maeneo mahsusi kwa ajili ya ufugaji lakini pia kutunza vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na katika Halmashauri ya Kilwa kama nilivyotangulia kusema tayari bajeti imeandaliwa ya milioni 60 kwa ajili ya kupitia mipango bora ya ardhi. Zoezi hili ni endelevu mpaka tutakapokamilisha vijiji vingine vilivyobaki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili kuhusiana na ongezeko la wananchi ni kweli wafugaji wengi wamehamia Kilwa na Mkoa wa Lindi kwa ujumla na baadhi ya mikoa mingine. Serikali inaendelea kufanya tathmini na kuona maeneo yale ambayo yana wafugaji wengi basi tuweze kuweka mgawanyo sahihi ili kulinda mazingira lakini kuepusha migogoro, ahsante.