Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 105 2023-02-08

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi ili kuondoa migogoro ya Wakulima na Wafugaji katika Wilaya ya Kilwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa ina jumla ya vijiji 90 na kati ya vijiji hivi, vijiji 56 vina Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi mpaka kufikia mwaka wa fedha 2021/2022.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuondoa na kumaliza kabisa migogoro ya wakulima na wafugaji ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara, Serikali imejipanga kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi ya vijiji sita kwa kila mwaka. Aidha, kwa mwaka huu wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 60 kwa ajili ya kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi ya vijiji vitatu vya Nandete, Kiranjeranje na Ruhatwe na kufanya urejeaji wa mipango ya matumizi ya ardhi iliyokwisha muda wake katika Vijiji vya Kandawale, Likawage na Nanjilinji B.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukabiliana na changamoto hizo, halmashauri zote za wilaya nchini zimeelekezwa kutenga fedha kila mwaka katika bajeti zao kwa ajili ya kuandaa mipango ya matumizi ya ardhi kwenye maeneo yote ya vijiji ikiwa ni pamoja na kuweka alama zinazoonekana kwa urahisi ili kuwezesha maeneo hayo kulindwa na kuzuia mwingiliano wa kimatumizi unaofanywa na wananchi. Hatua hii itawezesha kumaliza migogoro ya ardhi inayohusisha wakulima na wafugaji, ahsante.