Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza: - Je, ni lini Serikali italeta sheria ya wamiliki wa vyombo vya usafiri kuwa na miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize maswali madogo mawili ya nyongeza. Kwanza nishukuru sana majibu ya Serikali, lakini sisi humu sote ndani wote ni watu wenye ulemavu watarajiwa na lazima tukiri kwamba mtu mwenye ulemavu hawezi kutoka point A kwenda point B kwa kutumia vyombo vya usafiri kwa sababu miundombinu haikidhi haja kabisa na katika jibu la Waziri amesema kwamba kuna TBS kuna LATRA ambao wanatakiwa kuangalia hivyo viwango;

Je, ni ipi sasa kauli ya Serikali kutoka na hili jambo ili watu wenye ulemavu na wenyewe wapatiwe haki ya msingi ya kupanda haya mabasi?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali langu la pili, watu wenye ulemavu wamekuwa wakinyanyapaliwa sana katika vituo vya mabasi na madaladala wakati wa kuingia katika hivi vyombo, kwa sababu kuna watu wasioona kuna watu ambao hawawezi kutembea unaona kwamba wanapata manyanyaso makubwa sana.

Je, ni utaratibu gani mzuri sasa ambao umewekwa kuhakikisha kwamba hawanyanyaswi na wanawekewa mpango mzuri wa kupanda katika hivi vyombo vya usafiri?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa balozi mwema wa watu wenye ulemavu. Kwa swali la kwanza anataka asikie kauli ya Serikali, kauli ya Serikali ni hii; kwanza natoa wito kwa wamiliki wote wa vyombo vya usafiri, daladala pamoja na mabasi na kwa kushirikiana na LATRA pamoja na TBS wahakikishe ya kwamba wanaweka miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuwanyanyapaa watu wenye ulemavu hususan katika maeneo ya stendi ama mabasi, hili tunatoa onyo kali sana kwa sababu watu wenye ulemavu ni binadamu kama binadamu mwingine yeyote na ahaki zote za msingi. Kwa maana hiyo, kupitia vyombo vyetu vya sheria na kupitia Jeshi la Polisi pamoja na TARURA pamoja na TANROADS kuhakikisha kwamba miundombinu yote wezeshi hususan barabara pamoja na mabasi kwa maana ya vyombo vya usafiri kwa wale wamiliki tunaweza kuhakikisha hivyo vinawekwa vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nisisitize hapa suala la kisheria kwa mtu yeyote atakayeonewa, tutahakikisha tunachukua sheria kali sana na itakuwa fundisho kwa watu wengine wote wanaonyanyapaa na kuwanyasa watu wenye ulemavu.