Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa adhabu kali kudhibiti vifo vya akina mama vinavyosabishwa na waume au watoto wao?

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Ninaomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza;

Kwa kuwa watuhumiwa wa matukio haya wanaachiwa huru kwa kigezo kwamba ushahidi haujapatikana.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuimarisha kitengo cha ushahidi na uchunguzi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, nini mpango wa Serikali wa kuzuia mauaji haya ili kuwanusuru wanawake hawa? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, maswali madogo mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza linaonesha kwamba kumekuwa na muda mrefu wa kesi hizi zikiwa na visingizo vya kupatikana kwa ushahidi wa haraka. Kesi za mauaji zina utaratibu wake katika upelelezi wake. Walio wengi wanafikiri ni jambo la mara moja katika kufikia maamuzi ya upelelezi unaohusisha mauaji, lakini kwa namna yeyote ile muda uliowekwa na mahakama na vyombo vya upelelezi umekuwa ukizingatiwa sana katika masuala ya kesi hizi za mauji na hivyo hatuna kumbukumbu sahihi za watu ambao wamekaa magerezani muda mrefu kuliko kile kipindi ambacho tumekiweka kama dhamirio la kuwapa nafasi wapelelezi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu namna ya kuzuia mauaji haya; hili ni jambo la kijamii. Mambo haya mengi yamekuwa yakitokea kwenye jamii zetu na sisi wanajamii ndio tunastahili kuyakemea maana ni maisha yetu ya kila siku ambayo yanasababisha mauaji haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nipende tu kumpa maelezo muuliza swali; ni kwamba si mauaji tu kwa kina mama na watoto ukienda pale Njombe, nimetembelea Gereza la Njombe, asilimia 75 ya akina mama waliopo mle jela wakisubiri hizo kesi wanahusishwa na mauaji ya kuwaua waume zao. Kwa hiyo unaweza ukaona jinsi ambavyo mauaji haya yanajiografia zake; na mengine yote haya yanayojitokeza kweye jamii zetu wakemaji namba moja lazima tuwe sisi wenyewe wanachi katika maeneo yetu.

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa adhabu kali kudhibiti vifo vya akina mama vinavyosabishwa na waume au watoto wao?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa kwa miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la matukio ya wanafunzi kupewa adhabu kali ya viboko shuleni inayosababisha majeraha, kuzimia, kulazwa na hivyo kushindwa kuhudhuria shule ipasavyo.

Je, Serikali haioni ipo haja ya kuweka adhabu kali kwa waalimu wanaofanya vitendo hivi ili kuwalinda watoto wetu shuleni?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nipenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ongezeko la adhabu zisizo na kiasi kwa wanafunzi kule shuleni, na kwamba anaomba adhabu kali zitolewe kwa waalimu wale ambao wanachukua sheria mkononi; kimsingi limekuwa ni tatizo. Kila siku naona kwenye mitandao hatua ambazo walimu wanachukua. Mimi niwasihi, hasa walimu, kwa sababu tunayo sheria ya elimu inayotoa utaratibu wa adhabu kwa watoto wetu. Pale mtu anapochukua sheria mkononi atashtakiwa kama mhalifu mwingine yeyote ambaye ametumia nguvu katika kutoa adhabu kwa watoto wetu.