Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 6 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 101 2023-02-07

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa adhabu kali kudhibiti vifo vya akina mama vinavyosabishwa na waume au watoto wao?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Kanuni ya Adhabu imeweka adhabu ya kosa la mauaji ya kukusudia kuwa ni kunyongwa hadi kufa. Aidha, kwa makosa ya mauaji bila kukusudia Mahakama inaweza kutoa adhabu nyingine yoyote kulingana na mazingira na namna kosa lilivyotendeka. Hata hivyo kwa kosa la mauaji ya bila kukusudia sheria imeweka adhabu ya juu ya kifungo cha Maisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, Adhabu ya Kunyongwa hadi kufa ndiyo adhabu kali kuliko zote hapa nchini pamoja na ulimwenguni kote. Ahsante.