Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kutumia Pori tengefu la Mabwepande kama chanzo cha mapato?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa shughuli zote zilizotajwa ambazo zimeanza kufanyika ndani ya Pori la Akiba la Mabwepande, tayari wananchi wengi hawajui na hata wananchi wa Jimbo la Kibamba pia hawajui;

(a) Je, Serikali ipo tayari kufungua geti upande wa Jimbo la Kibamba ili wananchi wengi sana waweze kushiriki kwenye shughuli zilizotajwa kwenye jibu la msingi?

(b) Kwa kuwa katika kila uwekezaji tunategemea mapato na seerikali imejibu hapa imeshatumia shilingi 710,789,122. Je, ni yapi makadirio ya mapato katika mwaka 2022/2023?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Issa Mtemvu Mbunge wa Kibamba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, pori hili la Mabwepande ni pori ambalo limepekena na Mikoa jirani ikiwemo Pwani na pori hili lipo katikati ya Dar es salaam, kwa sasa tumeshaanza kufanya hamasa mbalimbali na kwa kuwa mwanzoni tulikuwa hatuna miundombinu tumeweza sasa kuwekeza na sasa hivi tuna miundombinu ya kutosha na hivyo watalii wameshaanza kuingia na matamasha mbalimbali yameshaanza kufanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshaanza pia kutumia mitandao ya kijamii kuhamasisha wananchi, pia tunatumia televisioni matamasha mbalimbali kama ambavyo nimeyataja ikiwemo nyama choma festival hii yote ni kuwafanya wana Dar es salaam wawe na maeneo maalum ya kupumzika ikiwemo kulala ambapo tumeshaandaa maeneo ya camp site kwa ajili ya wananchi kulala.

Mheshimiwa Naibu Spika, naendelea kuhamasisha Watanzania wote unapofika Dar es Salaam basi tembelea Pori la Pande utapata huduma zote za kiutalii na utaweza kuwa umepumzika kama vile upo Serengeti National Park.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye upande wa mapato tangu tulipowekeza katika pori hili kwa sasa tumesha kusanya jumla ya shilingi milioni 4.9 na kwa kuwa uwekezaji ni endelevu tunaendelea kuwekeza ili kuhakikisha kwamba eneo hili linakuwa ni kivutio kikubwa katika mkoa wa Dar es Salaam. (Makofi)