Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 6 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 97 2023-02-07

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutumia Pori tengefu la Mabwepande kama chanzo cha mapato?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Jimbo la Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha Pori la Akiba Pande linaendelea kuwa kitovu cha utalii katika Jiji la Dar es Salaam na maeneo jirani kuwa chanzo cha mapato, Serikali imetumia kiasi cha shilingi 710,789,122 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya utalii zikiwemo public camp site Mbili katika eneo la Msakuzi na Jomeke na Picnic Site Mbili eneo la Bwawani na Crater pamoja na ujenzi wa uzio wa bustani ya wanyamapori.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi hiyo imekamilika na imeanza kutumiwa na watalii ambapo kwa sasa shughuli mbalimbali zikiwemo mbio za Marathon, nyama choma festival, utalii wa kutembea kwa miguu na kuendesha baiskeli, upigaji picha na matamasha mbalimbali vimeanza kutumika.