Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kukomesha ukatili wa kijinsia nchini?

Supplementary Question 1

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Taarifa za Polisi na mambo tunayoyaona kila siku kwenye jamii yanaonesha kwamba ukatili wa kijinsia unaendelea kuongezeka; je, nini sababu ya ongezeko hilo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara imeweka mikakati mingi ya kudhibiti ukatili wa kijinsia ikiwemo Mabaraza ya Watoto, Madawati ya Jinsia, Kamati za Ulinzi, nani anaratibu afua hizi zote? Kwa nini basi tunapata taarifa tu kutoka kwenye Dawati la Polisi, lakini kwenye hizi afua mlizoweka hatupati taarifa zake? (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bernadeta, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli taarifa za Jeshi la Polisi zinaonesha kwamba ukatili umeongezeka. Sababu ya kuongezeka vitendo vya ukatili ni mmomonyoko wa maadili wa malezi na makuzi kwa Watoto; wazazi na walezi kutowajibika kumlinda mtoto; matumizi mabaya ya kieletroniki, na pia kuiga maadili ambayo siyo utamaduni wa Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe Waheshimiwa Wabunge wanapokuwa katika majukwaa yao kutoa elimu hii ya kutokomeza ukatili wa jinsia kwa wananchi wao. Vilevile tunaambiwa mtoto wa mwenzio ni wako, kwa hivyo tuwajibike sote.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Swali lake la pili, afua zote zinatekelezwa na Wizara tukishirikiana na wadau mbalimbali hasa Jeshi la Polisi ambalo lina mamlaka ya kutoa taarifa zote za ukatili wa kijinsia katika nchi yetu, ahsante. (Makofi)