Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 6 Community Development, Gender and Children Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum 94 2023-02-07

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukomesha ukatili wa kijinsia nchini?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maendeleo ya Jamiii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bernadeta Kasabago Mushashu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili wa Kijinsia unaozingatia kuimarisha uchumi wa kaya, kutokomeza mila na desturi zinachochea ukatili, kuimarisha malezi na makuzi na kusimamia sheria na kuwezesha huduma kwa waathirika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati za Ulinzi wa Wanawake na Watoto zimeundwa kuanzia ngazi ya Taifa hadi Kijiji. Zinafanya kazi zake katika Halmashauri kuhusu kutokomeza ukatili. Vituo vya Jeshi la Polisi, Magereza na Madawati ya Jinsia, Vyuo na Sehemu za Umma wanaunda madawati ya jinsia, Shule za Msingi na Sekondari zinaunda Madawati ya Ulinzi wa Watoto. Vilevile, Kampeni za kupinga ukatili zinaendelea sambamba na hatua za kuboresha sheria mbalimbali, ahsante.