Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, ni lini BOT itashusha riba inapokopa kupitia Hati Fungani kufikia asilimia 10 ili wananchi waweke fedha kwenye Benki za Biashara?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Pia niipongeze sana Serikali kwa kupunguza riba katika hati fungani kwenye level tofauti. Ningependa kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika swali la kwanza; kwa sababu sasa hivi Serikali inafungua uchumi, inafungua nchi na kila mtu anatakiwa ashiriki katika suala zima la uchumi. Je, Serikali inaonaje kwamba ipunguze idadi ya minada ya hati fungani kusudi mabenki ya biashara yaweze kufanya biashara yaweze kupata wawekezaji, ili tuweze kuongeza mzunguko wa fedha nchini?

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili; ningependa kuiomba Serikali miaka saba iliyopita Serikali ilikuwa inapitisha fedha zake kwenye mabenki ya biashara na zile fedha zilikuwa zinakaa pale muda mrefu, kwa hiyo kulikuwa na mzunguko mkubwa wa fedha na wananchi walikuwa wanaweza kukopa na hata riba zilikuwa zimepungua kwa sababu kulikuwa na fedha nyingi kwenye mabenki ya biashara. Je, Serikali haioni muda umefika sasa wa kufungua tena kwamba fedha zake ziwe zinakaa kwenye mabenki ya biashara kusudi wananchi waweze kukopa, mzunguko wa fedha uongezeke lakini pia na riba ziweze kushuka?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. David Mathayo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kupunguza idadi ya riba katika hati fungani ni swali la kisheria, lakini Serikali imelichukua na tutalifanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Dkt. Mathayo alileta ombi kwamba minada iwe inapungua mwenendo wake wa riba, basi nalo Serikali imelichukua na tutalifanyia kazi.