Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 6 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 88 2023-02-07

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: -

Je, ni lini BOT itashusha riba inapokopa kupitia Hati Fungani kufikia asilimia 10 ili wananchi waweke fedha kwenye Benki za Biashara?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, viwango vya riba za hati fungani vilifanyiwa marekebisho mwezi Aprili 2022 ambapo hati fungani ya miaka 25 ilishuka kutoka asilimia 15.95 hadi 12.56; Miaka 20 kutoka asilimia 15.49 hadi 12.10; Miaka 15 kutoka asimilia 13.5 hadi 11.15; Miaka 10 kutoka asilimia 11.44 hadi 10.25; Miaka saba kutoka asilimia 10.08 hadi 9.48; Miaka mitano kutoka asilimia 9.18 hadi 8.6; na miaka miwili kutoka asilimia 7.82 hadi 7.6. Riba za hati fungani zilishushwa ili kuendana na riba za soko na pia wananchi waweze kuweka fedha zao kwenye benki za biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, wastani wa riba za hati fungani za Tanzania zipo chini ikilinganishwa na Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afika Mashariki. Aidha, Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania itaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa riba za hati fungani za Serikali na kuchukua hatua stahiki ili kutoathiri akiba za fedha katika benki za biashara, ahsante.