Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isianzishe madawati ya kijinsia katika ngazi za Kata na Vijiji kutokana na ongezeko la vitendo vya ukatili?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza nasikitika kwa majibu ya Serikali, kwa sababu tunatambua kwamba ukatili wa kijinsia umeongezeka, sasa mpaka leo wanatuambia madawati ya kijinsia yako 420 na tuna kata takribani 4000. Ina maana takribani asilimia 10 tu ndio watu wanaopata hii huduma ambao wana athirika. Hata hivyo madawati ambayo wanasema wanatarajia kuanzisha Mashuleni wameanzisha so far, Madawati 1,300 na tuna shule zaidi ya 30,000 kwa Sekondari na Msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kamati hizi anazodai kuamzishwa kwa asilimia 88, aidha hazijaanza kazi labda kwa sababu ya changamoto ya kimuundo au kibajeti. Nataka kujua sasa, ni lini Serikali itazielekeza halmashauri ziweze kutenga bajeti ili kuhakikisha kwamba zinazipatia hizi kamati ambazo zimeanzishwa kwenye hivi vijiji ili ziweze kutekeleza kwa tija na kupunguza au kuzuia kabisa matukio ya ukatili wa kijinsia ambayo yamekithiri katika jamii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, kwa sasa matukio haya ukatili wa kijinsia yanakuwa hayachukuliwi hatua mpaka pale labda vyombo vya habari au mitandao ya kijamii inapo ripoti kwenye jamii ndipo tunaona viongozi wa ngazi za juu wanafuatilia na kuchukua hatua. Nilitaka kujua Serikali imeweka utaratibu upi ambao utawezesha utolewaji wa taarifa na ufuatiliaji wa matukio ambayo yameripotiwa kwenye hizi kamati ambazo mmesema zimeanzishwa kwa asilimia 88 ili kuhakikisha…

MWENYEKITI: Mheshimiwa uliza swalo sasa.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Ndilo swali lenyewe, ili kuhakikisha sasa waathirika wa vitendo vya ukatili wanapata huduma na haki staki kwa wakati?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther ifuatvyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na Halmashauri kutenga fedha kwa ajili ya kuimarisha kamati. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Esther kwa wazo zuri ambalo amelitoa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe waheshimiwa Wabunge ambao wanaingia katika Mabaraza ya Madiwani walipe kipaumbele suala hili ili Kamati hizi ziweze kujiwezesha na baadaye kufanya kazi kwake kwa makini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mifumo na utoaji wa taarifa. Kwa suala hili kwa kuwa utekelezaji wa MTAKUWWA ni mtambuka, Serikali itaendelea kutumia mifumo iliyopo kisheria. Kuhusu swali la Jeshi la polisi ndio muamala ambao unaweza kutoa taarifa za ukatili wakati upelelezi unapo kamailika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili Mwananchi aweze kuhukumiwa, Mahakama ndiyo itakayo toa hukumu katika vifungu ambavyo vilivyowekwa. Hata hivyo kesi ili iende haraka tunawaomba waathirika wote wawe na ushirikiano na vyombo vya sheria na pia kuwa wawazi katika kuleta maelekezo yao. Ahsante. (Makofi)

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isianzishe madawati ya kijinsia katika ngazi za Kata na Vijiji kutokana na ongezeko la vitendo vya ukatili?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu ya Mheshimiwa Waziri ameonesha kwamba asilimia 88 ndio wameunda katika vijiji, kata na kwenye mitaa yetu. Hata hivyo Kamati hizi zimekuwa hazitekelezi majukumu yake ama hazifahamiki ipasavyo. Mimi nilitaka kujua, je, kamati hizi za ulinzi na usalama wa watoto zimeundwa na wajumbe gani ili tuwatatmbue tuweze kuwafuatilia?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swal la nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwongozo wa Kuanzishwa Madawati ya Ulinzi na Usalama kwa Watoto ulianzishwa Juni, 2022 na kuanzishwa madawati hayo machache. Hata hivyo wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Wizara ya Elimu pamoja na Mamlaka ya Jeshi la polisi tutaendelea kuimarisha Kamati hizi ifikapo mwaka 2023 basi tutahakikisha shule zote zina madawati. (Makofi)

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isianzishe madawati ya kijinsia katika ngazi za Kata na Vijiji kutokana na ongezeko la vitendo vya ukatili?

Supplementary Question 3

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa matukio ya ukatili wa kijinsia yameendelea kukithiri hapa nchini, je, ni lini Serikali italeta Muswada wa Sheria ya Ukatili wa Kijinsia hapa Bungeni kama ambavyo Tanzania iliridhia katika Mkutano wa 44 wa Bunge la SADC (SADC Parliamentary Forum)?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Mbunge, tutajipanga Wizara pamoja na Wizara mtambuka ambazo tunatengeneza miamala hii ya miswada kwa pamoja ili kuweza kuifikisha pale panapohitajika, ahsante sana.