Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Community Development, Gender and Children Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum 85 2023-02-06

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: -

Je, ni kwa nini Serikali isianzishe madawati ya kijinsia katika ngazi za Kata na Vijiji kutokana na ongezeko la vitendo vya ukatili?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maendeleo ya Jamaii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholus Matiko Mbunge wa viti maalumu kama ifuatvyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kudhibiti vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii ambapo imeratibu uanzishwaji wa madawati 420 ya Jinsia katika vituo vya Jeshi la Polisi, na 153 vya Jeshi la Magereza. Aidha, madawati ya ulinzi wa watoto yameanzishwa katika shule za msingi na sekondari. Vile vile, madawati ya jinsia yanaanzishwa kwenye vyuo vyote nchini pamoja na maeneo ya umma kama kwenye masoko. Kwa upande mwingine, kKamati za Ulinzi wa Wanawake na Watoto zimeanzishwa katika ngazi ya mtaa/vijiji hadi Taifa kwa asilimia 88. Madawati haya yanachangia kwa kiasi kikubwa katika kushughulikia masuala ya ukatili wa kijinsia katika jamii. Ahsante