Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU K.n.y. MHE. ABDULLAH ALI MWINYI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa taarifa ya utekelezaji wa Blueprint for Regulatory Reforms za mwaka 2018 ili zijadiliwe?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Ninalo swali dogo tu la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mpango huu wa blueprint ulitengeneza changamoto mbalimbali ambazo ziko kwenye Sheria mbalimbali na ucheleweshaji katika kuushughulikia imekuwa ni issue. Wizara ina mpango gani sasa kwamba makosa mapya hayajirudii kwenye sheria zinazotengezezwa mpya?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Olelekaita kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli moja ya changamoto katika mambo yaliyokuwa kwenye andiko hili la blueprint ilikuwa ni Sheria na Kanuni zipatazo 88 ambazo zilikuwa na changamoto mbalimbali. Mpaka sasa zaidi ya Sheria na Kanuni 40 zimeshafanyiwa kazi ambayo ni takribani asilimia 45 ya utekelezaji ya mpango huu wa kuboresha mazingira ya wafanya biashara nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tunaendelea kupitia na kuhakikisha Sheria na Kanuni ambazo bado ni kinzani kwa ajili ya kuweka mazingira bora ya ufanyaji biashara nchini tunaendelea kuzitatua na kupitia Bunge lako Tukufu ninaamini mengi tutaendelea kuyarekebisha kadri ya muda unavyokwenda, kwa sababu pia tunavyotatua baadhi ya changamoto kuna changamoto zingine mpya zinaibuka. Kwa hiyo, Serikali itaendelea kutatua kadri ambavyo hali halisi itakavyokuwa inajitokeza.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU K.n.y. MHE. ABDULLAH ALI MWINYI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa taarifa ya utekelezaji wa Blueprint for Regulatory Reforms za mwaka 2018 ili zijadiliwe?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na maelezo aliyoyatoa Mheshimiwa Naibu Waziri, tumekaa hapa tunaongea lakini huko Halmashauri zetu wanatunga Sheria Ndogondogo ambazo zilizopo nyingi zinakwenda kupunguza attraction ya wawekezaji hasa wa ndani.

Je, ni mkakati gani wa sasa ambao Wazira inao kuhakikisha inaratibu zoezi hili ili liweze kuhakikisha kwamba Wawekezaji hasa wa ndani wanaweza wakafanya kazi bila ya kuwa na Sheria Ndogondogo hasa za tozo?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Deo Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli moja ya changamoto tulizonazo kwenye utekelezaji wa mradi wa blueprint au MKUMBI ni katika ngazi za Halmashauri. Wizara tumeshaanza kuliona hilo na moja ya utekelezaji tumeanzisha madawati au kitengo mahususi kinachoshughulikia masuala ya viwanda, biashara na uwekezaji katika ngazi ya Halmashauri. Tunaamini kitengo hiki kitasaidia moja, kuhakikisha tunaharakisha utekeklezaji wa yale maboresho ambayo tumeyafanya, lakini pili kuwaelimisha wenzetu wa Halmashauri ili wawe wanatunga Sheria au Kanuni ambazo si kinzani na nia hii ya Serikali ya kuboresha mazingira ya uwekezaji na ufanyaji biashara hapa nchini. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU K.n.y. MHE. ABDULLAH ALI MWINYI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa taarifa ya utekelezaji wa Blueprint for Regulatory Reforms za mwaka 2018 ili zijadiliwe?

Supplementary Question 3

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ni nchi ya 141 kati ya 190 kwa ugumu wa ufanyaji biashara. Majibu ya Mheshimiwa Waziri yananipa mashaka juu ya commitment ya Serikali juu ya kutumiza haja ya reforms katika regulations zetu. Hivi ni kwa nini hiyo taarifa ya utekelezaji msiilete Bungeni ili tuweze kuijadili, badala ya kuipeleka kwenye Kamati peke yake, tuleteeni Bungeni hapa tuijadili, tuna usongo na hali hii sisi, tunataka tumalize haya matatizo. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Abbas Tarimba Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ya Kudumu ya Viwanda, Biashara na Mazingira, ni moja ya Kamati ambazo zimetungwa na Bunge lako Tukufu. Kwa hiyo namini kwa utaratibu ule ule kwamba Kamati hizo zinawasilisha Bunge hili na kwa maelekezo yenu nadhani inawezekana kama kutatakiwa kuleta hapa, basi ni maelekezo ya Bunge lako Tukufu ili tuweze kufanya hivyo.

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU K.n.y. MHE. ABDULLAH ALI MWINYI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa taarifa ya utekelezaji wa Blueprint for Regulatory Reforms za mwaka 2018 ili zijadiliwe?

Supplementary Question 4

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mpaka sasa hivi Blueprint inaonekana ni document ya Serikali na watu hawaimiliki. Ni yapi sasa mafanikio mpaka sasa hivi tangu tufanye reforms kwenye blueprint, Serikali imefanikiwa nini kiuchumi ili at least sasa tuanze kuona value for money na hayo marekebisho ambayo tumeyafanya?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Nusrat Hanje, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mafanikio yako mengi kama ambavyo nimesema. Moja ya maeneo ambayo yalikuwa yana angaliwa ni zile Sheria zilizoanishwa kwenye mpango ule au kwenye document hiyo, ambayo kimsingi iko public na kila mtu anaweza ku-access na sio ya Serikali. Ni zaidi ya sheria na kanuni 88, ambazo katika hizo sheria na kanuni 40 zimeklwisha ratibiwa na kufanyiwa marekebisho. Hata hivyo katika mambo ambayo yalikuwa yameibuliwa ni mwingiliano kati ya taasisi za Serikali moja wapo mi TBS na TMDA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo mengi yameweza kurekebishwa; lakini moja ni uanzishwaji wa mifumo ambayo ilikuwa na changamoto kwa wafanyabiashara kwa mfano Wafanyabiashara wakitaka kulipia ilikuwa ni changamoto kubwa. Kwa hiyo mifumo 42 imerekebishwa, moja wapo tunaona ni hii GEPG ambayo ni malipo ya Serikali na yameboreshwa na hii imepunguza sana manung’uniko kwa wananchi kupanga foleni Kwenda kulipa katika taasisi mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi katika utekelezaji huo ndiyo tunaona kwamba tumeanzisha idara hizi na vitengo ambavyo vitakuwa mahususi sasa kusikiliza na kutatua kero za wafanyabiashara maeneo yote. Kuanzia wizarani kuna kitengo hicho lakini pia tunaenda kwenye halmashauri tunaweka kitengo ili kuhakikisha tunapunguza manung’uniko na changamoto ambazo wafanyabiashara wa Tanzania walikuwa wanakutana nazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo taarifa hizo au kitabu hicho au document hiyo ni ya wananchi wote. Kwa hiyo popote utakapotaka unaipata na taarifa hizi kama ulivyosema kama ukihitaji tutaileta hapa Bungeni; lakini Kamati yako ya Viwanda, Biashara na Mazingira wamekwisha ipata na wameijadili na mambo mengi yanaendelea kurekebishwa.