Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 5 Investment and Empowerment Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 84 2023-02-06

Name

Abdullah Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mahonda

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU K.n.y. MHE. ABDULLAH ALI MWINYI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa taarifa ya utekelezaji wa Blueprint for Regulatory Reforms za mwaka 2018 ili zijadiliwe?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdullah Ali Mwinyi, Mbunge wa Jimbo la Mahonda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilianza rasmi utekelezaji wa mpango wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini (MKUMBI) ujulikanao kama blueprint hapo Julai Mosi, 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kulifahamisha Bunge lako Tukufu kwamba tarehe 24 Oktoba, 2022, Wizara iliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa MKUMBI kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira. Katika taarifa hiyo ambayo inaonesha utekelezaji wa hadi kufikia Agosti, 2022 ilijadiliwa, ambapo Kamati ilitoa maelekezo mbalimbali ya kufanyiwa kazi ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa mpango huo, maelekezo hayo yanaendelea kuzingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru.