Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE.ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa REA II utamalizika kwa Vijiji 25 vilivyobakia katika Jimbo la Rungwe?

Supplementary Question 1

MHE. ANTON A. MWANTONA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitoe masikitiko yangu makubwa, nimekuja mara nyingi hapa kwa mradi wa REA II ambao ni Vijiji 25, ukizingatia huu mradi ulikuwa ni mradi wa mwaka 2014 ndiyo ulianza, hivi vijiji 25 vilitelekezwa. Nilikuja hapa mwaka jana mwezi wa Februari Bunge, Naibu Waziri mwenyewe hapa alisema kwamba Mwezi April mradi utakuwa umeshakamilika. Nimekuja Bunge la Mwezi wa Sita akaniambia mwezi wa Tisa mradi utakuwa umeshakamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekutana na Waziri mwenyewe amekuja kufanya ziara kule nyumbani Jimboni kwangu, amefanya mkutano na wananchi pale Tukuyu akawaambia mpaka Disemba mradi utakuwa umeshakamilika. Leo hii naambiwa hapa kwamba mradi huu umechanganywa na REA Namba III Awamu ya Pili na utaisha Disemba, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda Wizara haikuelewa vizuri swali langu. Huu ni mradi REA II ambao ni wa muda mrefu, nilikuwa naomba nipate majibu. Ni lini mradi wa REA II vijiji 25 utakamilika?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, REA III Awamu ya Pili nilikuwa na Vijiji 36, mpaka ninavyoongea hapa ni Vijiji Vitatu tu ndiyo vimeshawashiwa umeme, kuna Kijiji cha Mboyo Kata ya Isongole, Kijiji cha Ndwati na Kijiji cha Lienje Kata ya Ikuti na deadline ilikuwa ni Disemba mwaka 2022. Leo naambiwa hapa kwenye swali la msingi kwamba tunapeleka tena mpaka Disemba 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nafikiri ni lazima tuwe serious kwa sababu wananchi wetu wanatusikiliza, ahadi Serikali wanazotoa nasi tunawaambia, leo naambiwa 2023 ndiyo mradi utakamilika. Naomba nipate ufafanuzi wa Serikali, mambo gani yaliyopelekea kubadilisha deadline kutoka Disemba 2022 mpaka Disemba 2023?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anton Albert Mwantona kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama swali lilivyoulizwa ilikuwa ni kwamba ni lini Vijiji vilivyobaki katika REA II vitakamilishwa. Kule mwanzo vilipochukuliwa hivi Vijiji 25 vilitakiwa vifanyike katika REA II lakini havikufanyika vilibaki. Kwa sababu maelekezo ya Serikali ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ni kwamba hii Awamu ya REA III mzunguko wa pili usiache kijiji hata kimoja bila kupelekewa Umeme. Kwa hiyo, Vijiji hivi 25 vimeunganishwa kwenye Mkataba wa REA III Round II ili navyo vifanyiwe kazi na vikamilike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupanga ni kuchagua tutawaelekeza wenzetu wanaotekeleza mradi kwenye maeneo haya ili wahakikishe kwanza katika scope hii wanashughulika na vile Vijiji ambavyo ni vya muda mrefu halafu hivi ambavyo vilikuwa ni vya REA III Round II waje wavimalizie kwa kadri tunavyosogea mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lingine ambalo ni la msingi ameuliza kuhusu kubadilika kwa muda wa kumaliza mkataba wa REA III Round II kutoka Disemba mwaka jana kwenda Disemba mwaka huu. Sababu kubwa ziko mbili, kwanza ni ile ambayo tulikwisha ieleza ya matatizo tuliyoyapata ya kuongezeka kwa bei na changamoto zilizotokana na UVIKO, tatizo jingine ni tatizo chanya ambalo ni kuongezeka kwa Kilometa Mbili kwa kila Kijiji katika mradi huu ambao unaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo kwa scope ile ya zamani ambayo ilitakiwa iishe Disemba, baada ya kuongeza zaidi ya nusu ya ile scope imekwenda sasa kufikia mpaka Disemba mwaka huu, tutahakikisha kwamba tutavutana na kukabana na Wakandarasi ili hizi kilometa mbili ambazo zinaongezeka kwenye Vijiji vyetu Disemba mwaka huu kazi yote iweze kukamilika katika maeneo yetu.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE.ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa REA II utamalizika kwa Vijiji 25 vilivyobakia katika Jimbo la Rungwe?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo langu la Arumeru Magharibi wananchi wanahitaji umeme kwa asilimia 100. Kuna Mkandarasi ambaye yupo kwenye Jimbo hilo ambaye amekuwa akisuasua kuwapa wananchi umeme, kuna maeneo kuna maeneo amechimba mashimo, hakuna nguzo kwa muda mrefu, kuna maeneo ameweka nguzo hakuna nyaya kwa muda mrefu, maeneo mengine hakuna umeme kabisa....

MWENYEKITI: Sasa uliza swali lako Mheshimiwa.


MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Jimbo la Arumeru Magharibi ambao wamesubiri umeme wa REA kwa muda mrefu bila mafanikio?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lemburis Noah Saputi, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo ambayo tulichelewa kupata Mkandarasi eneo la Arumeru ni mojawapo, Mkandarasi tayari amepatikana na anaendelea na kazi, katika maeneo ambayo tunaangalia kwa macho ya Karibu Mkoa wa Arusha pia ni mmojawapo. Tunahakikisha kwamba katika muda ambao tumekubaliana nae wa kimkataba kazi yake ya kupeleka umeme kwenye maeneo hayo itakamilika. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tunaomba atupe subira kidogo na utatuona sana katika Jimbo lake tukiendelea kuvutana na Mkandarasi kuhakikisha kwamba kazi inakamilika katika muda tuliokubaliana.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE.ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa REA II utamalizika kwa Vijiji 25 vilivyobakia katika Jimbo la Rungwe?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Kwa kuwa tatizo la usambazaji wa umeme kupitia Wakandarasi wa REA III mzunguko wa pili imekuwa tatizo kubwa katika Majimbo yetu. Je ,Wizara haioni umuhimu sasa wa kutusikiliza Kikanda kuona matatizo yalivyo kwenye Majimbo yetu katika mradi huu wa REA?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swalil la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto zilikuwa nyingi, zile za ndani ya uwezo na nje ya uwezo. Changamoto zilizo ndani ya uwezo zote tumeshazitatua. Siku chache zilizopita Mheshimiwa Waziri aliitisha kikao cha Wakandarasi wote na kutoa maelekezo, tayari wenzetu wa REA wameshapita kwenye Mikoa takribani Saba au Nane ambayo tuliona iko nyuma zaidi kuhakikisha kwamba wao, watu wa REA na watu wa TANESCO kwa kushirikiana na Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa lakini na Waheshimiwa Wabunge pia mlipata mialiko kwenye hayo maeneo tukae kwa pamoja ili tuone tatizo liko wapi na tuweze kusukuma shughuli hii ili tuweze kuikamilisha kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumewekeana makubaliano na tunaamini ndani ya muda tutayatekeleza na tutakamilisha kazi hizo.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE.ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa REA II utamalizika kwa Vijiji 25 vilivyobakia katika Jimbo la Rungwe?

Supplementary Question 4

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaona REA wanayo miradi mbalimbali lakini tunaotoka Majimbo ya Mjini na tunayo mazingira ya maeneo ambayo yana sifa za vijiji ingawa yako Mjini. Je, ni lini mtatupelekea umeme kwa sababu hata miradi hakuna huko, tunaona tu ya REA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano Iringa Manispaa mtaa wa Ugele, Mtaragara, Msisina, Kagrielo na Wahe, ni lini mtatuletea umeme maeneo ya pembeni?(Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jesca Msambatavangu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu wenye Majimbo ya Vijijini wamekuwa na miradi ya REA na densification na mingine, sisi ambao tuko kwenye Majimbo ya Mjini na mimi nikiwemo Jimbo la Bukoba Mjini, tumepata mradi unaoitwa peri-urban ambao kama nilivyotangulia kujibu kwenye siku zilizopita, mradi huu sasa umeenda kwenye awamu ya pili na tutakwenda kwenye awamu nyingine zinazokuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ilianza Mkoa wa Pwani na Kigamboni, awamu ya pili ikaja Mkoa wa Arusha, Dodoma na Mwanza, Awamu ya tatu imepata Mikoa mingine kama mitano au sita, sasa tutaenda awamu ya nne nimhakikishie Mheshimiwa Msambatavangu kwamba na Iringa pia itaingia kwenye awamu inayokuja kwa sababu pesa inapatikana taratibu lakini kila mmoja lazima apate pesa katika kufanya miradi hii kwenye maeneo yake.